2018-05-18 16:36:00

Mabaraza mawili yatoa Waraka mpya "Oeconomicae et pecuniariae quaestiones"


Waraka mpya wa Baraza la Kipapa la Mafundisho Tanzu ya Kanisa na Baraza la Kipapa la Maendeleo endelevu ya Binadamu umepewa jina la “Oeconomicae et pecuniariae quaestiones” ambao una kusanya mawazo kwa ajili ya mang’amuzi ya maadili katika baadhi ya mantiki ya sasa kwenye mfumo wa uchumi na fedha. Na katika utangulizi ambao unaelekeza Waraka huo mpya wa “Oeconomicae et pecuniariae quaestiones, wanaandika kuwa “Dhana ya kiuchumi na fedha kwa ajili ya maendeleo katika njia ya ustawi wa binadamu uwe  halisi na endelevu. Inapaswa kufungamana wazi katika msingi wa maadili na lazima kuonekana kati ya ufahamu kiufundi na hekima ya binadamu”.
 
Waraka huo umekubaliwa na Baba Mtakatifu  Francisko na  kutangazwa kwa wote. Pamoja na kutangzwa umewakilishwa kwa vyombo vya habari Vatican na Kardinali Peter Turkison Baraza la Kipapa la Maendeleo endelevu ya Binadanadamu pamoja na  Kardinali Ladaria, Mwenyekiti wa Barza la Kipapa la Mafundisho Tanzu ya Kanisa . Katika waraka huo, unaonesha vipengele mbalimbali msingi kama vilivyo fafanuliwa kwa kirefu kama vile: Upendo wa wema kamili ni ufunguo wa maendeleo; ulimwengu unaotawaliwa na mantiki zilizokwisha wakati;  kuchuma na kufaidika binafsi ni maombolezo; uchumi na utamaduni wa ubaguzi; tabia za  ubinafsi zinafanya kulipa gharama kubwa kwa wote; mitindo mipya ya uchumi na hatimaye kipengele cha mwisho ni kile cha  kutafuta wema wa pamoja.

Upendo wa wema kamili ni ufunguo wa maendeleo: Katika kujikita kwenye Wosia wa Laudato Si wa Papa Francisko, Waraka huu wanasititiza kuwa, upendo wa jamii na juhudi za kutafuta wema wa pamoja zinaundwa kwa mtindo wa upendo ambao hautazami tu mahusiano kati ya mtu, badala yake ni mahiusiano ya ulimwengu, mahusiano ya kijamii, kiuchumi  na kisiasa.Ufunguo wa maendeleo ya dhati ni upendo wa wema wa pamoja ambao hauteni na upendo kwa ajili ya ukweli. 
Na ili kuweza  kuhamasisha maendeleo hayo ni ngumu hasa kwa upande wa mang’amauzi ya kimaadili. Na Kanisa linatambua kati ya kazi yake msingi ambayo inawaalika wote kwa unyenyekevu wa uhakika katika baadhi ya mantiki msingi 
 
Ulimwengu unaotawaliwa na  mantiki zilizokwisha wakati wake: Katika Waraka mpya unatathimini pia hata historia  ya hivi karibuni ambayo inajikita katika uchumi duniani. Kipeo cha sasa cha fedha , kingeweza kuwa fursa ya maendeleo na uchumi mpya zaidi katika umakini wa maandili msingi na katika utaratibu mpya wa kuratibu shughuli za fedha kwa kuyeyusha zile mantiki ya wizi na uchunguzi wakati hyo huo kuweza  kuthaminisha zaidi huduma ya uchumi wa sasa.  Lakini pamoja na juhudi chanya katika ngazi mbalimbali kwa bahati mbaya umekosekana uhusiano mwema na ukaleta matokeo yaliyofikia kufikiria mantiki ambazo zinaendelea hadi sasa kutawala dunia!

Kuchuma na kufaidika binafsi ni maombolezo:Matukio ambayo hayakubariki ni yale ambayo yanatokana na kuchuma na kunyonya vilevile kuendelea kunufaika binafsi  na kujitajirisha  pasipo kufaidisha wengine, kwa maana hiyo ni kuunda wasiwasi katika ustawi wa walio wachache au wakati  wakati mwingine uchumi unatawaliwa na kushushwa bei ziweze chini na ambazo zinasabaisha  kupanda kwa  madeni mengi ambayo yanawakilisha matokeo hasi katika hali halis ya nchi nyingi.

Uchumi na utamaduni wa ubaguzi: Pamoja na hayo hata wasiwasi juu ya mantiki ya uchumi ndiyo Papa Francisko anaitafsiri, “utamaduni wa ubaguzi” Katika Waraka unathibitisha kuwa, ni mchezo wa kweli wa ustawi watu katika sehemu kubwa ya watu wanaolia katika sayari hi ina ambao wako hatarini, wameachwa pembezoni mwa jamii bila kuwa na maendeleo  yoyote kwasababu ya kunyonywa malighafi na utajiri wote ardhini mwao.
Ubinafsi unafafanya kulipa wote gharama kubwa: KatikaWaraka huo inaonesha ulazima wa kufikiria kwa upya mitindo ya uchumi kutokana na ukosefu wa kugawana sawa.  Kwa maana hiyo wanasema imewadia sasa wakati wa kufikiria kwa dhati kibindamu na kupanua upeo wa akili na moyo, kwa kuwa na utambuzi wa hali halisi kwa kile kinacho fikia katika dharua ya kweli na wema.

Mitindo mipya ya uchumi: Wataalamu na wahusika wanaalikwa kwa namana ya pekee kushirikiana katika mitindo mipya ya kiuchumi na fedha mahali ambapo mchakato na utaratibu viweze kuweka katika maendeleo endelevu kwa wote, kuheshimu hadhi ya binadamu, uhakika wa zana za mafundisho jamii ya Kanisa. Hata hivyo hata ule ulazima wa kuanza kwa upya kutafakari juu ya mantiki  za kuwa wawakili wa fedha   ambao unatambua kusimamia na kufanya kazi kwa maana mara baada ya kutenguka kwa msingi ya maadili na maandili ya binadamu ndiyo unasababisha matokeo ya ukosefu wa haki sawa vile vile kuonekana kwa mfumo mbaya ulio undwa ana ambao unazidi kutmika duniani.

Kutafuta wema wa pamoja: Ili kuweza kuratibu vema mifumo ya sasa ya kiuchumi na fedha, kila mmoja anaweza kufanya  mambo mengi sana, hasa iwapo hakuna ubianfsi na kujitenga kwa maana vipo vyama vingi vya kiraia ambavyo  vinawakilisha kwa maana nyingine, utunzaji wa dhamiri njema na uwajibikaji kijamii. Leo hii kama zamani, waraka unahitimishwa na kusisitiza kila mmoja anaalikwa kuwa makini kukesha kama walinzi wa maisha bora na kutafsiri kwa upya wakiwa mstari wa mbele kijamii katika matendo haid na thabiti kutafuta wema wa pamoja ambao unajikita katika misingi imara ya mshikamano na kugawanya wa usawa wa pamoja
 
Sr Angela Rwezaula 
Vatican News!








All the contents on this site are copyrighted ©.