Makatekista wote wa nchi wanapaswa kujifunza vema juu ya siasa ya utetezi na ulinzi wa watoto iliyokubaliwa na maaskofu mnamo mwaka 2017. Habari zilitozotolewa na Shirika la habari za kimisionari fides wanathibitisha kuwa Padre Jovin Riziki Mkurugenzi wa ofisi ya huduma za kijamii wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC amethibitisha kuwa katika kazi nzuri iliyofanywa na Kanisa, hasa katika utangulizi kwa mantiki ya dini kati ya watoto, maaskofu wanaonesha wajibu wa kila mtu kuendeleza uwezo na kujifunza vema juu ya siasa ambayo inalinda na kutetea kwa namna ya kufikia watu wengi katika utoaji wa nyenzo msingi za kusimamia na kuwalinda watoto. Padre Riziki amethibitisha hayo wakati wa hotuba yake katika semina ya siku tatu uliyoandaliwa na Sekretarieti ya jimbo kuu kwa ajili ya makatekista na semina hiyo imemalizika hivi karibuni, kurasini jijini Dar Es Salaam Tanzania.
Wakati wa hotuba hiyo, Padre Riziki pia ameongeza kusema kwamba hata Waziri wa
Afya ameagiza kuwakilisha mpango mzima juu ya utetezi na ulinzi wa watoto, uliokubaliwa
mwaka jana na maaskofu wa nchi katika ofisi yake, mpango ambao unapaswa kujikita katika
matendo ya dhati hasa kwa wale wanao fanyakazi ndani ya Kanisa Katoliki na wale ambao
wanajikita na shughuli ya ufundishaji shuleni na vituo vya kulea na kutunza yatima.
Kwa maana hiyo ni lazima kuwasaidia wengine mafunzo kama hayo katika majimbo juu ya
kuanzishwa kwa shughuli hii ya maaskofu katoliki nchini Tanzania.
Katika semina hiyo pia hawakukosa kujita kwa kina kuhusiana na mada nyeti sana inayohusu
vitendo viovu na vihalifu dhidi ya watoto, na jinsi gani watoto wengi wanaathirika
kisaikolojia, kihisia, hata kijinsia, suala nyeti ambali linazidi kuongezeka ndani
ya jamii. Siasa hiyo ni wazi, kwa maana kila anayejiingiza katika ukatili wa kijinsia
dhidi ya watoto, lazima ahukumiwe.Kati ya lengo madhubiti na msingi la maaskofu
katoliki Tanzania, ni lile la ulazima wa kuanzisha ofisi kwa ngazi ya kitaifa na
kijimbo, kwa maana ya kwamba, masuala yote yanayohusu manyanyaso ya wadogo yaweze
kukabiliwa kwa kina. Zaidi Padre Riziki amehitimisha akisema, shule zote zinapaswa
kuwa na mwakilishi na mwakili wa kulinda na kutetea watoto, ili kuweza kung’amua wale
ambao wana athiri wadogo na habari hizo ziweze kufika Parokiani au katika ofisi ya
mkurugenzi wa jimbo anayehusika na utetezi wao kwa ufanisi wa kukabiliana na tatizo.
Sr Angela Rwezaula
Vatican News
All the contents on this site are copyrighted ©. |