2018-05-03 15:35:00

Miaka 50 ya Chama cha Kitume cha Wakatekumeni Wapya mjini Roma!


Tarehe 5 Mei 2017 Njia ya Ukatekumeni Mpya unafanya mkutano mkubwa wa kimataifa huko Tor vergata jijini Roma na Baba Mtakatifu Francisko katika furaha ya maadhimisho ya miaka 50 tangu chama hicho kikanyage mguu wake Roma, mara baada ya kuanzishwa mjini Madrid nchini Uhispania mwishoni mwa mwaka 60. Katika fursa hiyo Baba Mtakatifu atawabariki na kuwatuma wanajumuiya 34 ya ""Missio ad gentes na Jumuiya 25 za chama hicho katika umisionari kwenye parokia za pembezoni mjini Roma. Mkutano na Baba Mtakatifu Francisko utaanza saa 5 masaa ya Ulaya lakini saa 4 kamili wataanza na utangulizi kutoka kwa Kiko Argüello, mwanzilishi wa kimataifa katika hatua hizo cha chama cha kitume cha wakatekumeni wapya.

Eneo lilochanguliwa kufanyika mkutano ni sehemu ya Chuo Kikuu cha Tor Vergata, kando ya mji wa Roma kwa ajili ya kumuenzi Mtakatifu Yohane Pauli II ambaye kwa miaka 26 kama Khalifa wa mtume Petro aliwakaribisha na kuwasaidia mchakato wa hatua za chama hiki cha kitume cha wakatekumeni wapya. Na ikumbukwe, Tor Vergata ndiyo mahali ambapo waliadhimisha Siku ya Vijana duniani Mwaka 2000 ikiwa ni Jubilei ya Ukristo ! Kutokana na maombi ya maaskofu wengi, mitume wapya amvao ni mapadre 34  wa missio ad gentes wataweza kubarikiwa na kutumwa ili wapeleke Injili katika maeneo mengi yaliyomezwa na malimwengu au sehemu ndogo ya uwepo wa Kanisa katika miji duniani kote.
 
Baba Mtakatifu pia atawabariki na kuwatuma jumuya 25 za wakatekumeni wapya katika maparokia ya Roma  ambao tayari wamefanya hatua za mchakato wa  hatua za ukristo, hata katika parokia nyingine pembezoni mwa Roma, mahali ambapo maparoko wameomba msaada ili kusaidia wengi ambao wako mbali na imani. Mkutano wao utahitimishwa  na sala ya  wa shukrani, “Te Deum”, ikiwa na maana ya kushukuru Mungu kwa miaka 50 tangu kufika mjini Roma chama cha kitume  hiki. Maombi ya shukrani yataongozwa na kikundi cha kimataifa cha wakatekumeni wapya. Pamoja na hayo watamkumbuka kwa namna ya pekee hata Carmen Hernández, mwanzilishi msaidizi mwenzake wa  Kiko wa chama cha Kitume cha wakatekumeni wapya aliyerudi kwa baba mbinguni mnamo tarehe 19 Julai 2016.

Sr Angela Rwezaula 
Vatican News!








All the contents on this site are copyrighted ©.