Kama alivyo kuwa ametangaza, Baba Mtakatifu taarifa kuhusu siku ya Mei Mosi mchana kuazana mwezi wa Bikira Maria kwa kutembelea Madhabahu ya Bikira Maria huko “Divino Amore” kando ya mji wa Roma kuungana na waumini wengine kusali Rosari kwa namna ya pekee kwa ajili ya nchi ya Siria na Dunia nzima, amehitimisha hija hiyo jioni ya Mei Mosi! “Tusali kwa pamoja kwa ajili ya amani nchini Siria” ndiyo wito wa Papa Francisko aliowaomba maelfu ya waamini waliofika katika Madhabahu ya mama Maria wa Divino Amore, Roma.
Ni maelfu ya waroma waliompokea Papa Francisko katika uwanja mbele ya Mnara wa
Muujiza wa kwanza katika Madhabahu ya Mama Maria wa Divino amore, dakika chache kabla
ya kufika saa 11 majira ya jioni masaa ya Ulaya. Baba Mtakatifu amechangua mwaka huu
kuanza mwezi wa Maria kwa hija katika madhabahu inayopendwa sana na watu wakazi wa
Roma. Kabla ya kuingia katika Madhabahu ya zamani ili kusali Rosari Takatifu, amewasalimi
waamini waliokuwa wamekusanyika katika uwanja na kuwomba wamfuatile wakiwa pale kusali
Rosari.
Wakati akiingia katika madhabahu ya zamani mbele ya Picha ya Mama Maria wa miujiza,
msomaji alikuwa akiendelea kusoma wito wa amani kwa ajili ya nchi ya Siria. Ni maneno
yaliyo tamkaBaba Mtakatifu wakati Sikukuu ya Pasaka, kama utamaduni wa kutoa baraka
ya Urb et orbi mbele ya Kanisa la Mtakatifu Petro Mjini Vatican.
Pamoja na waamini wote ambao tayari walipata nafasi katika Madhaahu ndogo ya zamani,
wamesalia rosari ya matendo ya uchungu. Baada ya Sala ya Rosari, Baba Mtakatifu amerudi
kiwanjani mahali ambapo maelfu ya watu walikuwa wakimsubiri na ambao wamesali naye
wakiwa kwa nje. Na kwa njia hiyo Baba Mtakatifu amesali Sala ya Salam Maria na baadaye
kuwabariki na kuanza safari ya kurudi Vatican.
Ziara ya Baba Mtakatifu siku ya Mei Mosi katika Madhabahu ya Bikira Maria wa Divino
Amore, imesindikizwa na Askofu Mkuu Angelo de Donatis, makamu mkuu Askofu wa Roma,
Askofu Paulo Lojudice Msaidizi wa kitengo cha Roma kusini, Monsinyo Enrico Feroci
, Mkuu wa Shirika la Waoblati wa Wana wa Mungu Upendo, Padre Luciano Chagas, Gombera
wa Madhabahu hiyo, Padre Vincent Pallippadam Gombera wa Seminari ya Maria wa Divino
Amore na Paroko Padre John Harry Bermeo Sanchez.
Sr Angela Rwezaula
Vatican News
All the contents on this site are copyrighted ©. |