2017-12-22 09:02:00

Kipindi cha mwisho cha Baba Yetu,Papa amesema,inahitaji ujasiri kutamka Baba


Katika kipindi cha mwisho cha tafakari ya “Baba yetu”  Kipindi ambacho kimeongozwa na Padre Marco Pozza, ambaye ni Padre Mhudumu wa gereza la wafungwa huko Padua,  kwa kawaida mfululizo wa  vipindi vyote 8 vimekuwa na wageni waalikwa,ambao ni ulimwengu wa walei waliobobea kwenye masuala ya utamaduni wa taifa pamoja na usanii mbalimbali, ambao walikuwa wakizungmza  mara baada ya utangulizi wa Baba Mtakatifu kwa sala hiyo ya Baba Yetu.

Kwa njia hiyo Jumatano usiku wa tarehe 20 Desemba 2017 kilikuwa ni kipindi cha 9  katika mfululizo wa Sala ya Baba Yetu. Kipindi hiki kilianzishwa kwa ushirikiano wa Sekretarieti ya Mawasiliano Vatican na  Kituo cha luninga Tv2000 kinachomilikiwa na kuendeshwa na Baraza la maaskofu nchini Italia.
Katika vipindi hivyo  “Padre nostro”, katika kuenzi sala ya Baba yetu na maisha ya sala kwa mkristo, Kipindi kilikuwa  na sehemu tisa, ambacho kimerushwa  kila Jumatano, majira ya saa 3 na dk 5 kwa saa za Ulaya. 

Baba Mtakatifu akichambua Baba yetu na Padre Marco Pozza  kwa kipinchi cha tisa na cha mwisho amendelea kusema kuwa , tunasema kuwa sisi ni wakristo na tunasema kuwa tunaye baba, lakini tunaishi, kana kwamba, ndiyo hasemi kama wanyama, lakini kama vile watu ambao hawaamini katika Mungu na katika binadamu, wanaishi  bila imani na kuishi tukitenda mabaya, hatuishi kwa upendo bali kwa chuki, katika mashindano na katika vita.
Baba Mtakatifu anauliza maswali, je Mungu anatukuzwa kati ya watu wanao pambana kati yao kwa ajili ya mali? Je anatukuzwa  katika maisha ya wale ambao wanafanya mipango ya kiahalifu, ili kuweza kumwondoa adui? Je anatukuzwa katika maisha ya wale ambao hawawatunzi vema  watoto wao? Hapana, Baba Mtakatifu amesisitiza  kuwa, Mungu hawezi kutukuzwa jina lake kwa namna hiyo!

Mafundisho ya Maneno ya Yesu yanatoa mwangwi katika matukio na maisha ya Baba Mtakatifu Francisko katika wito wake wa kitume, na hasa kujikita katika mahangaiko na matumaini ya wanawake na waamini wa sasa , hadi kuweza kugeuka kuwa na maisha yenye utajiri wa maana na lengo.
Na kwa maana hiyo, Baba Mtakatifu anabanisha kuwa inahitaji ujasiri wa kusalia sala ya Baba yetu. Inahitaji ujasiri wa kujiweka tayari kutamka  “Baba” na kuamini kweli kwamba Mungu ni Baba yetu ambaye ananisindikiza, ananihurumia , ananipatia mkate na kuwa makini kwa kile ambacho mimi ninaomba na ananivalisha vizuri zaidi ya maua ya kondeni . Kuamini hata hivyo ni ni tendo la kujiweka katika hatari na wasiwasi, kwa maana unajiuliza maswali mengi kwamba, je ni kweli ninacho kiamini? . Lakini Baba Mtakatifu anathibitisha kuwa ni vema kujaribu kuamini. Na ndiyo maana ni vizuri kabisa kusali kwa pamoja, kwa maana tunasaidiana mmoja baada ya mwingine.

Baba Mtakatifu Francisko pia  ametoa mfano wake binafsi kwamba,zamani walipokuwa watoto wadogo , walifundishwa kuwa mkate ulikuwa wa dhììthamani kubwa na ulipokuwa unaanguka, ilikuwa lazima kuookota , kuubusu na kuula. Kwa maana hiyo, mkate ni ishara ya umoja wa binadamu  na ni ishara ya upendo wa Mungu kwa ajili yako anayekupatia mkate huo. Akiendeleza kufafanua juu ya historia hiyo binafsi, amesema, mikate iliyokuwa inabaki wakati wa kumaliza  kula, bibi na mama walikuwa wakifanya nini? Waliifadhi vema na baadaye walichanganya na maziwa na kutengeneza keki au kitu kingine, lakini kamwe mkate haukutupwa.

Halikadhalika amesimulia tukio jingine kuwa, siku moja huko Buonos Aires ilifika Sanamu ya Mama yetu wa Fatima ikiwa inazungushwa na ambapo waliandaa misa ya wagonjwa katika uwanja mkubwa  wa mpira ambao ulikuwa umejaa sana. Wakati huo Askofu alikwenda kuungamisha, na aliungamisha kabla ya Misa na baada ya Misa. Baba Mtakatifu anasema,  mwisho hapakuwapo na watu maana walikuwa wote wametawanyika na kurudi makwao,  wakati anakaribia kuamka, ili aondoke  kwa maana alikuwa anasubiriwa sehemu nyingine ili kuweza kutoa kipaimara,alifika mwanamke mmoja mdogo. Huyo mwanamke alikuwa rahisi pia alikuwa amevaa nguo nyeusi utafikiri ni wanawake wakulima wa Kusini mwa Italia, ambao huvaa nguo nyeusi kipindi chote cha maombolezo.

Mwanamke huyo alikuwa na macho  mang’avu yaliyokuwa yakimulika uso wake, na ndipo Baba Mtakatifu aliuliza swali  kama alikuwa anataka kuungama, lakini akamwambia, “wewe hauna dhambi”. Mwanamke akamjibu kwa lugha ya kireno, “sisi sote tuna dhambi”. Kwa njia hiyo Baba Mtakatifu akasema, “kuwa makini: labda Mungu hasamehi” Mwanamke akajibu, “Mungu anasamehe kila kitu”…alijibu hayo  kwa uhakika. Baba Mtakatifu akauliza “Je wewe unajaje?” mwanamke akajibu “ Kama Mungu hasamehi yote, dunia isingekuwapo”. Baba Mtakatifu Francisko ameongeza kusema kuwa wakati huo alitaka kumwambia hivi wewe umesoma Chuo Kikuu cha Gregoriana!. Kwa mwaana hiyo Baba Mtakatifu amemalizia kwa kuthibitisha kuwa hiyo ni hekima ya watu rahisi,wanaotambua kuwa Baba yetu daima anawasubiri.

Ikumbukwe,  katika makutano, maneno na majibu ya Baba Mtakatifu na Padre Marco Pozza, kimetolewa pia  kitabu cha Baba yetu "Papa Francisko", kinachopatikana kwa sasa katika maduka ya vitabu mjini Vatican.

Sr Angela Rwezaula
Vatican News

 








All the contents on this site are copyrighted ©.