Baada ya misa Takatifu ya kutoa daraja Takatifu la Upadre kwa mapadre wapya 16, naye Kardinali Patrick D’Rozario, Askofu Mkuu wa Dhaka, ametoa hotuba yake fupi ya kumshukuru Baba Mtakatifu Francisko ya kuwa,anapenda nchi ya Bangladesh, kwa maana ameonesha hivyo kwa njia nyingi. Na upendo wake mwingi uliojaa furaha ya kichungaji katika zizi dogo umeoneshwa katika kuwakilishwa na wakristo walio kusanyika kutoka pembe za nchi nzima na kwa njia hiyo wanatoa shukrani kubwa!
Akisimulia juu ya eneo hilo, Askofu Mkuu amesema kuwa, uwanja uliotumika kuadhimisha misa Takatifu umejaa hostoria, kwani ni mahali ambapo Baba wa Taifa, Bangabandhu Sheikh Mujibur Rahman, alitoa hotuba yake tarehe 7 Machi 1971, wakati nchi ya Bangladesh inajitangazia uhuru wake. Kwa njia hiyo, hata leo hii kwa mara ya kwanza wakristo wote wamepata kuadhimisha Ekaristi Takatifu, ili kuenzi mchango wa kumbukumbu ya eneo hilo la kihistoria na kwa namna ya pekee ni ishara kubwa na heshima ya nafasi maalumu iliyo nayo Kanisa iliyo katika nchi hiyo.
Halikadhalia Askofu Mkuu Rozario amesema, Papa wa kwanza kufika katika ardhi hiyo, alikuwa ni Mwenye heri Papa Paulo VI, Novemba 1970 ili kuonesha upendo wake na huruma kwa waathirika waliokumbwa na mafuriko, yalisababishwa vifo karibia milioni moja ya watu. Na kwa njia hiyo hiyo Kardinali anamkubusha Papa kuwa, kama ilivyotokea kwa mtanguliz wake kufika katika tukio hilo, hata yeye amependelea kufika katika nchi hiyo ili kuonesha mshikamano wa upendo, ukaribu na ukarimu kwa wale wahitaji.
Sr angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |