2017-10-15 15:44:00

Papa ametangaza Sinodi ya Maaskofu Oktoba 2019 kwa ajili ya Amazon


Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya kuadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, Jumapili tarehe 15 Oktoba 2017 kwa ajili ya kuwatangaza watakatifu wapya waliotetea imani yao hadi kufikia mauti, amewashukuru  waamini na watu kutoka mataifa mbali mbali waliokuwapo katika  Ibada Kuu ya kuwatangaza Watakatifu wapya. Kwa namna ya pekee, amewakumbuka wawakilishi maalum kutoka nchini Brazil, Ufaransa, Italia , Mexco, Kisiwa cha Malta na Uhispania. Baba Mtakatifu anasema, kwa maombezi ya mashahidi wa mwanga wa Injili , waweze kutusindikiza katika safari  na kusaida kuhamasisha daima mahusiano ya kindugu, mshikamano  kwa ajili ya Kanisa na jamii.

Aidha anasema, katika kupokea  maombi ya baadhi ya Mabaraza ya Maaskofu wa Amerika ya Kusini pia sauti mbalimba kutoka kwa wachungaji na waamini  kutoka baadhi ya pande za dunia, ameamua kuitisha Sinodi maalum ya maaskofu wa Makanisa za Panamazon, Sinodi itakayo fanyika Roma mwezi Oktoba 2019. Lengo msingi wa kuitisha Sinodi hii, Baba Mtakatifu anathibitisha kuwa,  ni kuweza kuchanganua njia mpya za uinjilishaji kwa zile za watu wa Mungu wa asili, ambao daima wamesahaulika na kukosa msimamo wa sasa  na nyakati endelevu na utulivu. Baba Mtakatifu anaongeza, hiyo inatokana na kipeo cha msitu wa Amazon ambacho ni kiini  cha mtaji muhimu katika sayari yetu. Kwa njia ya Watakatifu wapya wasaidie maombi kwa ajili ya tukio hilo la Kanisa ili kwa heshima ya uzuri wa uumbaji, watu wote duniani wamsifu Mungu Bwana wa ulimwengu na katika  mwanga wake waweze kutembea kupitia njia za haki na amani.

Vile vile Baba Mtakatifu amekumbusha kuwa, Jumanne tarehe  17 Oktoba 2017 ni  Siku ya Kupamba na Umaskini Duniani. Baba Mtakatifu anasema, umaskini siyo maafa nazo sababu  zake ambazo ni lazima kutambuliwa na kuondolewa ili kuheshimu hadhi ya ndugu kaka na dada wengi kwa mfano wa hawa watakatifu.

Sr angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.