Baba Mtakatifu ametoa ujumbe wake kwa njia ya video kutokana na maadhimisho ya miaka 300 ya kupatikana kwa Sanamu ya Bikira Maria wa Aparecida nchini Brazil. Na katika tukio hili BabaMtakatifu amemteua Kardinali Giovanni Battista Rei Mwenyekiti mstaafu wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Maaskofu na Mwenyekiti mstaafu wa Baraza la Tume kwa ajili ya nchi za Amerika ya Kusini kumwakilisha katika maadhimisho ya miaka 300 ya kupatikana kwa sanamu ya mama yetu wa Aparecida, ambaye ni msimamizi wa nchi ya Brazil, sikukuu inayofanyika katika Madhabahu ya Kitaifa ya Aparecida kwa siku kuanzaia 10-12 Oktoba.
Katika ujumbe wa video anaanza na salamu kwa watu wote kuanzia viongozi wote wa
Kanisa, na serikali ya nchi ya Brazil wanaotoa ibada ya Mama Yetu wa Aparecida na
msimamizi wa Brazil. Baba Mtakatifu anatoa salam zake na baraka maalumu kwa wote wanaoishi
na Kristo katika Jubileia ya mwaka wa Maria kushehereka miaka 300 ya kupatika kwa
sanamu ya mama huo kutoka katika mto wa Paraíba do Sul.
Katika tukio la ziara yake ya kwanza ya ya kitume kimataifa mwaka 2013 , Baba Mtakatifu
anasema alipata furaha na neema ya kutembelea Madhabahu hayo na kusali mbele ya sanamu
ya Mama Maria akimkabidhi utume wake wa kipapa na kukumbuka watu wa Brazil kwa makaribisho
yao mema na moyo wao wa ukarimu. Katika tukio hilo, Baba Mtakatifu anaongeza kuwa,
alionesha upendeleo wa kusheherekea nao Jubilei hiyo, lakini maisha ya kuwa papa anasema
siyo rahisi.
Kwa njia hiyo anasema amemtuma mwakilishi wake, Kardinali Giovanni Battista Re aweze kuadhimisha sherehe hizo tarehe 12 Oktoba 2017. Yeye amemkabidhi utume huo wa kuhakikisha uwepo wa Baba Mtakatifu karibu nao. Aidha anasema pamoja na kutokuwapo kimwili,kwa bahati nzuri anaonesja shuhuku hiyo kwa njia ya Mtandao wa Mawasiliano wa Aparecida kuonesha ukarimu na upendo wa watu hao wenye ibada kuu ya Mama wa Yesu ambapo Baba Mtakatifu anatoa maneno rahisi yenye kutaka kuwakilisha uwepo wake kindugu katika sikukuu hiyo.
Akirudia maneno aliyo ya tamka mbele ya altare ya Madhabahu ya Kitaifa mwaka 2013 huko Aparecida , “tufungie na kutunza matumaini ili Mungu aweza kutoa mshangao na kuishi kwa furaha. Matumaini, kwa watu wa Brazil ni fadhila ambayo inapaswa kujikita zaidi katika mioyo ya wale wote wanao amini na zaidi hasa katika kipindi kigumu na misukosuko na mahali ambapo ni kujisikia kukata tamaa. Baba Mtakatifu anawashauri kuwa, wasikubali kukata tambaa , wasikubali kushindwa, wawe na matumaini kwa Mungu,na matumaini kwa Mama yetu wa Aparecida, Baba Mtakatifu anasisitiza. Katika madhabahu ya Aparecida na kila mwenye ibada ya Maria wote wanaeweza kuonja matumaini yanayo imarisha katika uzoefu wa kiroho, ukarimu , mshikamano, uvumilivu, na katika undugu, katika furaha vitu ambavyo ni vyenye thamani kubwa katika maisha na kujikita kwa undani mizizi yenye nguvu ya imani ya kikristo.
Katika mwaka 1717 kipindi ambacho wavuvi majini walikumbana na Sanamu ya Mama
Maria wa Aparecida , baba Mtakatifu anaongeza, pale walihisi kuwa na imani kwa Mungu
ambaye anatoa mshangao kwetu daima. Samaki kwa wingi na neema zilizotawanyika kwa
namna halisi ya maisha ya wale ambao walikuwa wanamtegemea dhidi ya wenye nguvu. Mungu
anatoa mshangao kwasababu ni yeye aliye tuumba kwa upendo upeo na anatushangaza
daima. Katika kushereherekea jubilei ya miaka 300 ambapo Mungu anatoa mshangao , wote
wanaalikwa kuwa na furaha na shukrani.Furahisni katika Bwana daima (Fil 4,4). Furaha
hiyo itokayo ndani ya mioyo yao inaweza kufikia kila kona ya nchi ya Brazil hasa katika
maeneo ya pembezoni, kijamii na kuishi, kwa wale ambao kila wakati wanayo shahuku
ya kuonja hata tone la matumaini hayo.
Tabasamu rahisi la Mama Maria wanayojaribu kuiona katika uso wa picha, iwe ndiyo
chemichemi ya tabasamu ya k la mmoja mbele ya matatizo ya maisha. Mkristo kamwe hawezi
kuwa mgumu!
Anamalizia ujumbe huo akiwashikuru watu wote wa Brazil kwa ajili ya sala zao za kila siku anazo mwombea hasa wakati wa maadhimisho ya misa, anasisitiza waendelee kusali kwa ajili yake, kama vile yeye anavyosali kwa ajili yao , kwa maana wote wawe karibu au mbali wanaunda Kanisa na watu wa Mungu . Na kila wakati wanaposhirikiana kwa pamoja hata kwa njia rahisi lakini kwa dhati ni kutangaza Injili, ni kugeuka kuwa mashuda, kuwa wafuasi wa kweli na wamisionari. Leo hii nchi ya Brazili inahitaji wanaume na wanawake wenye kujawa na matumaini na imani thabiti, wawe mashuhuda wa upendo na kuonesha mshikamano, katika kushikirikishana na mambo yenye nguvu na mwanga katika giza la ubinafsi na ufisadi. Anawabariki na baraka ya kitume kwa maombezi ya Mama yetu wa Aparecida.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |