2017-10-07 14:24:00

Kard.Koch: Umoja ni zawadi ya Roho Mtakatifu.Hakuna njia nyingine!


Umoja ni zawadi ya Roho Mtakatifu, kwa njia hiyo, uekumene ni njia muhimu ambayo inatokana na sala kwa  maana ni katika maombi ya pamoja, umoja huo unawezekana. Ni maneno yaliyo thibitishwa na Kardinali Kurt Koch Mwenyekiti wa Baraza ka Kipapa la Kuhamasisha umoja wa Kikristo, wakati wa kutoa hotuba yake katika Kanisa Kuu la Civitavecchia nchini Italia kwenye ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa mwaka wa Kichungaji katika majimbo tarehe 6 Oktoba 2017.

Akichambua kwa undani zaidi juu ya umoja wa  wawakristo, Kardinali Koch anatoa maelekezo ya historia ya mageuzi ya safari ya kiekumene, akianzia  katika Hati ya  pamoja ya Baba Mtakatifu Francisko na Askofu Younan Mwenyekiti wa Shirikisho la Makanisa ya kiluteri duniani uliotiwa sahini mwaka jana huko Sweden. Kwa upande  huo Kardinali anasema, mchakato huo unaweza kufikia umoja, hasa kwa upande wa wakatoliki kuanza kuwa na upeo chanya na mpya  juu ya mageuzi ya  Kanisa la Kiinjili. Upeo huo ni kutoa tofauti zilizokuwapo katika hali  ya wakristo wa mashariki ambao wamekabiliana nayo kwa miaka mini ya kale.

Kwa mujibu wa Kardinali, anasema hiyo inawezekana lakini , iwapo huruma na mapatano yanazingatia na kufuta mwelekeo msingi wa safari ya kiekumene endelevu. Aidha anafafanua kuwa pia inahitjai kuwa  na mtazamo wa mafundisho kuanzia katika Maandiko ya Mtakatifu na yale ya Mtakatifu  Agostino mwaka  1530, hata mengine yaliyofuata  yanayohusu  maungamo yake kwamba, muungano kamili wa kiekumene unawezekana kutokana na mabadiliko ya kudumu  ya Kanisa kwa njia ya Msingi Mkuu wa Injili na kutunza umoja wa Kanisa ambalo  linaungana  bila kutenganishwa.
Kardinali ameweza pia ujibu baadhi ya maswali kuhusiana na suala hili , ambapo amebainisha kuwa hakuna njia yoyote ya watu au mtaalamu wa mambo ya Mungu isipokuwa ni kwa njia ya uekumene unaofanya wakristo wote katika hali zote. Kwa njia hiyo anatoa mwaliko kwa kila mmoja kujenga,kuhamasisha, kuuliza na kujifuanza kutambua taalimungu ya Kanisa lake, kwa kushirikiana kindugu na Makanisa mengine, lakini kuficha kuwa matatizo yapo hasa yanayohusu mantiki ya mazungumzo ya pamoja.

Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.