2017-10-06 15:30:00

Papa:Haiwezekani kudharau hali ya utunzaji wa urithi wa Bahari yetu


Baba Mtakatifu ametuma barua iliyotiwa sahini na Kardinali Pietro Parolin Katibu Mkuu wa Vatican kwenye Mkutano  wenye kuhusu  mada juu ya “Bahari  yetu, ni bahari  kwa ajili ya maisha”. Ni mkutano wa siku mbili, tarehe 5 na Oktoba 2016 huko Malta. Ujumbe huo umewakilishwa na Askofu Mkuu Silvano Tomas , ambaye ni mwanachama wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Maendeleo ya Binadamu  aliyeshiriki katika kazi ya mkutano huo.
Katika ujumbe wa Baba Mtakatifu, anatia moyo  nguvu  na jitihada za kukabiliana na matatizo mengi ya haraka, kama vile biashara ya binadamu, utumwa, hali halisi zisizo za kibinadamu katika kazi ndani ya viwanda vya uvuvi na biashara ya usafirishaji. Aidha fursa za maendeleo ya jumuiya forodhani, familia za wavuvi  na hali ya kutisha katika visiwa vinaoshairiwa kukupotea kutokana na ongezeko la maji.

Bahari ni urithi wa pamoja katika familia ya binadamu, anaandika Baba Mtakatifu. Haiwezakani kudharau hali ya kutunza urithi huo dhidi ya   uchafuzi wa maji kwa njia ya platiki nyingi ambazo matokeo  yake ni mabaya ya afya na maisha ya binadamu anayefanya kazi baharini.
Kwa njia hiyo, Baba Mtakatifu anachukua  kipengele cha ujumbe wa Hati  ya “Sifa kwa Bwana” inayohusu  ulinzi wa Mazingira nyumba yetu.  Anasisitiza  kuwa, haiwezekani kuona wanapotea hata  baadhi ya viumbe majini  ambapo vinageuka kuwa makaburi ya viumbe majini visivyo kuwa na rangi ya maisha.
Baba Mtakatifu  anakumbusha jinsi asili ya kila kitu inavyohusiana  na kwamba, bahari zinaweza kuwa rasilimali  msingi katika kupambana na umaskini na mabadiliko ya hali ya hewa na kwamba,  hayo ni  matukio mawili ya karibu. Kwa njia hiyo   anabainisha kuwa hiyo ni kushindwa kwa mtu huyo  anayetumia bahari kwa ajili ya uharibifu, akitupa takataka na hutumiaji wa njia za kisasa za kumwaga uchafu wa tindikali utokanao na uchimbaji madini chini ya baharini.

Baba Mtakatifu katika kipengele kingine cha   ujumbe wa Sifa kwa Bwana anakumbusha umuhimu wa kuelimisha ushirikiano wa kibinadamu, mazingira ya pamoja, kuwafundisha vijana ili waweze kuwa makini katika hutoaji  wa huduma bora, pia kuwasaidia kukua katika ujuzi na kutafakari juu ya ukuu na ukubwa wake. Anamalizia akisema kwa muda mrefu sana, tahadhari imezingatia hali ya uhalifu na maafa ya kibinadamu baharini, bila ujasiri wa kutosha kukabiliana na sababu zake, ambazo mara nyingi zinapatikana kwenye ardhi. Ni wakati sasa wa kufanya kazi na wajibu mkubwa zaidi kulinda bahari zetu, nyumba yetu ya kawaida, na ndugu na kaka na dada zetu, leo na siku zijazo.


Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

       

 








All the contents on this site are copyrighted ©.