2017-09-29 16:38:00

Mahubiri ya Mons. Dario Vigano' katika Sikukuu ya Malaika Wakuu


Kila tarehe 29 Septemba Kanisa Katoliki linafanya sikukuu Malaika watatu walinzi nambao ni Mikaeli, Gabrieli na Raffaeli. Malaika Gabrieli ni msimamizi wa Radio Vatican, ambapo misa takatifu imeadhishwa katika Kanisa la Mtakatifu Maria wa Traspontina mjini Vatican. Katika misa hiyo Mwenyekiti wa Sekretarieti ya Mawasiliano Vatican ameadihmisha misa hiyo akiwa na mapadre wengine wa Radio Vatican.Kwenye  mahubiri yake anasema tunakutana pamoja katika altare kwa ajili ya kuadhimisha sikukuu ya msimamiz wa Radio Vatican Gabrieli pamoja na wenzake Michaeli na Rafaeli, mahali ambapo Kanisa limewaweka pamoja katika kufanya sikukuu ya wajumbe wa Mungu.

Uwepo wa mwanga katika roho za watakatifu hawa Malaika  inatusindikiza katika kusikiliza neno na kuumega mkate wa maisha. Monsinyo Vigano anauliza, Malaika ni nani?. Katika kujibu swali hili anasema, kulingana na Maandishi ya Matakatifu na mapokeo ya kanisa inatoa mitazamo miwili kuhusu malaika hawa. Kwa upande mwingine Malaika ni kiumbe hai mbele ya Mungu ambaye yupo mbele ya Mungu na mahali popote, kwa maana ya kwamba katika majina matatu ya malaika yanaishia na elufi ya EL maana yake ni Mungu, Mungu  ameandikwa katika majina yao maana ni asili yao. Asili yao ya kuishi ni uwepo kwa ajili ya  yake na tabia ya Malaika ni wajumbe wa Mungu. Wao wanapeleka ujumbe wa Mungu kwa watu. Kutoka kwa Mungu wanakaribia watu katika ardhi, wao hurudi kwa Mungu, kwa maana wao wanaisha daima na Mungu wakati huo huo wako karibu na binadamu.
Malaika wanaalikwa kutusindikiza sisi wenyewe, na  kufanya uzoefu wa ukarimu na upendo wa mungu ambaye anatukaribisha na kutukumbatia ili tuweze kuondona na udhaifu wa kila aina. Kwa njia hiyo anasema Monsinyo Vigano  tunagundua wito wetu  kuwa na sisi tunageuka kuwa  malaika kwa wengine, Malaika daima  anaongoza katika njia njema na kuepusha njia pofu

Hiyo ni wazi anasema kwasababu mapambano ni hali halisi ya kila siku kama ilivyoeleza somo la kwanza. Kwa maana aliye na shahuku ya kufuata Bwana lazima ipo kazi kubwa katika moyo katika maisha  familia, kazini , watu , katika jumiua zetu za Kanisa. Lakini Bwana ameweka karibu hivi viumbe vyenye mwanga ili giza la migogoro visiwe n anafasi ya kutishia na uzito wa mapambano usishinde furaha yetu. Wimbo wa mwisho katika  kitabu cha ufunuo , unasema,  Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni ikisema: “Sasa umefika ukombozi na nguvu na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake! Maana yule aliyewashtaki ndugu zetu mbele ya Mungu ametupwa chini. Naam, ametupwa chini huyo anayewashtaki usiku na mchana.(Ap 12,10).
Kitabu cha ufunuo ni cha aina yake kwa mana ni tukio linalijikita kila siku katika maisha yetu  na hasa inapotokea  kipindi cha kupambana kati ya mema na mabaya , mwanga na giza. Ni juhudi ambayo leo hii tunaalikwa kuchagua mema ambaye ni Kristo. Aliye tumia vema uhuru wake, na kupokea kwa huruma na msamaha wa baba yake kwa  njia ya damu ya mwanae akatufanya  hata sisi tuwe watoto wa Mungu.

Hatuna haja ya kuogopa anasema Vigano, kwasababu ubaya hautakuwa na neno la Mwisho. Injili inahakiki kwamba Yesu ndiye anayetupeleka kwa Baba ,kwa kupitia katika ngazi ya  msalaba wake , na zaidi ndiye yeye aliyesulibiwa. Kwa njia ya Yesu msulibiwa  Mungu anajionesha katika ardhi na kupaa mbinguni , Yeye ndiye daraja pekee  kati ya mungu na binadamu. Yote yanatokea kwa njia ya mwili wake na nyama yake iliyosubiliwa ili nasi tupate maisha.Katika matukio yetu, shughuli zetu na matatizo yetu Mosninyo Vigano anasisitiza, tumwachie yeye katika mwanga wa kweli na Mungu.Yeye Kamwe hatuachi pekeyetu na kusamehe pia.Hata sisi kama Malaika Gabrieli tunaweza kutangaza habari njema. Yeye alipeleka habari kwake Maria ya kwamba atakuwa mama wa Mtoto wa Mungu, alipeleka habari kwa Zakaria juu ya kuapzaliwa kwa Yohane.

Katika kazi yetu, tunaalikwa kusambaza habari njema ya ya maisha , uzuri, mshikamano na kushirikisha. Monsinyo Vigano ametoa onyo kuwa, inabidi kutambua kile ambcho tunatamka. La sivyo ni hatari kwamba tunapiga kelele ambayo haiwezi kuzaa matunda ya kusikiliza kwa dhati na hasa katika kusikiliza ziel  habari za kweli za mawasiliano. Hata sisi tunaalikwa kuwa malaika walio tayari kama Kristo ili kuweza kuishi ndani ya binadamu. Tunaalikwa kujitoa kushinda kila siku ya na kujiweka tayari katika ngazi zote zinazopelekea kukutana na Bwana , katika hali halisi ndogo ya kila siku. Ametoa mfano kuwa, Mwanamme kila siku anapanda ngazi kwa ajili ya mke wake, mama anatelemka ili aweze kupokea mwanae, aidha mgonjwa anakabiliana na ugonjwa wake. Kwa njia hiyo Baba Mtakatifu Francisko anatoa wito ,malaika ni roho wa utume  , waliotumwa kuhudumia wale ambao ni  warithi wokovu.Hivyo ni lazima kuwa na utambuzi wa uwepo wao japokuwa hawaonekani. Tuombe kila wakati kwa kukumbuka uwepo wa Mungu, watusindikize katika mapambano dhindi ya mabaya na kutufikisha katika njia ya hakika ya maisha yetu.

Sr Angela Rwezaula 
Idhaa ya kiswahili ya Radio Vatican

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.