2017-09-15 15:59:00

Vatican: Imefikia robo tatu Katiba ya mwongozo wa Kitume Vatican


Ni karibia asilimia 75 ya kazi ya kuchunguza Katiba ya mwongozi wa Kitume Vatican na mwisho wa mwaka huu  kutakuwapo na  uwezekano wa kuwasilisha nyaraka mpya kwa wanasheria wa Vatican. Ameyathibitisha maneno hayo katika vyombo vya habari vya Radio Vatican Kardinali Óscar Andrés Rodríguez Maradiaga, Askofu Mkuu wa Tegucicalpa (Honduras) ambaye ni Mratibu wa Baraza la Makardinali washauri wa Papa wakati wa kumalizia Mkutano wa 21 wa baraza hilo.

Shughuli za kitume katika mkutano huo si kwa ajili ya Baraza la Makardinali tu, bali pia ni lazima kujibu malengo ambayo Baba Mtakatifu Francisko amekabidhi.Kati ya masuala muhimu aidha amesema kuwa wanaamini kwamba baba Mtakatifu anayo matashi ya kutaka kuongeza zaidi wanawake na vijana ndani ya utume Vatican.Halikadhalika miongoni mwa mada zilizo jadiliwa katika Baraza hili jipya ambalo ni kama chombo cha uinjilishaji na huduma ambayo si  kwa ajili ya Papa bali hata kwa ajili ya Makanisa  mahalia ilikuwa:  ugawaji wa madaraka, nafasi ya ubalozi wa  Kitume, uteuzi na uwezo wa wafanyakazi, ambao wanapendelea wau wa kanisa wawe wachache zaidi lakini kuwajumuisha na wengi wa Kimataifa.

Naye Askofu Marcello Semeraro wa jimbo la Albano, nchini Italia ambaye ni  Katibu wa  Baraza la  Makardinali washauri wa Papa anathibitisha hayo kuwa mchakato wa mageuzi ya Vatican  umefikia sasa zaidi ya robo tatu na inatayarishwa kwa kiwango cha pendekezo la Baba Mtakatifu. Mkutano wa Baraza la Makardinali washauri wa Papa utafanyika  tena tarehe 11-13 Desemba 2017.
Naye Mkurugenzi wa  Habari za Vatican Bwana Greg Burke  ametoa habari zaidi juu ya Mkutano wa 21 wa Baraza la Makardinali washauri. Anasema Mkutano ulifunguliwa tangu jumatatu, kwa siku tatu uliudhuliwa na wajumbe wote japokuwa Kardinali George Pell na Kard. Laurent Monsengwo Pasinya hawakuwapo.

Akiongea na waandishi wa Habari, Bwana Burke ameweka bayana kuwa, Baba Mtakatifu ameshiriki na kundi hili kuanzia Jumanne asubuhi mara baada ya kutoka katika ziara yake ya kitume nchini Colombia, na hakuweza kuwapo Jumatano asubuhi kutokana na shughuli ya Katekesi yak ila Jumatano.
Kwa njia hiyo anasema, shughuli za Mkutano huo zilikuwa ni juu ya kusoma na kutafakari mapendekezo ya Baba Mtakatifu aliyotoa kwa Baraza hilo jipya. Pamoja na hayo kulikuwa na tafakari iliyoongozwa na Kardnali Óscar Rodriguez Maradiaga Mratibu wa Baraza hilo, kuhusiana na nyaraka mbalimbali za Papa juu ya mageuzi. Na hizo nyaraka hasa ni zile zitotokanazo na Mkutano wa jadi wa Papa na Jumuiya nzima ya Vatican aliotoa hotuba wakati wa kutoa matashi mema ya Krismasi, hotuba nyingine za mkutano Mkuu tarehe 12 Februari 2015, na 17 Oktoba 2015 wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya Sinodi ya Maakofu.

Sr Angela Rwezaula 
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.