2017-09-06 16:05:00

Barua ya Papa katika Mkutano wa Kimataifa wa Tasaufi ya Kiorthodox


Katika tukio la ufunguzi wa Mkutano wa  XXV wa Kimataifa wa Kiekumene wa tasaufi ya Kiorthodox, napenda kuwasalimia waandaji na washiriki wa Mkutano huo. Ni maneno ya utangulizi wa Baba Mtakatifu alio utuma Enzo Bianchi Mwanzilishi na Mkuu wa Jumuiya ya Wamonaki wa Monasteri ya Bose, ambao wameanza mkutano wa XXV wa kimataifa wa tasaufi ya  Waorthodox kuanzia tarehe 6 – 9 Septemba 2017 ukiwa na kauli mbiu “Ni zawadi kukuaribisha”.
Katika maneno ya Baba mtakatifu amemsalimia yeye binafsi na kwa namna ya pekee kiongozi wa Kiekumeni Patriaki Bartholomew na Theodros Patriaki wa Alessandria. Amesema uwepo wao ni muhimu katika Mkutano huo wa 25 katika Jumuiya ya Wamonaki Bozze kwa ushirikiano wa Makanisa mengine ya Kiorthodox ambayo inatoa thamani na mchango wa pamoja katika safari kuelekea katika umoja.

Kauli mbiu ya  mwaka huu inasema “ni zawadi  kukaribisha” kwa njia hiyo  inatia moyo na matumaini hasa katika hali ya sasa .Hakika kukaribisha ni zawadi; ni zawadi hawali ya yote tuliyoipokea pia sisi wote ni wageni katika ulimwengu,  sisi tulio umbwa na tunaopaswa kulinda. Pia sisi ni wasafiri katika ardhi hii na wageni wa ardhi hii; kwa njia kama  ni wageni  tunalikwa na kutarajiwa huko mbinguni, mahali ambapo kuna  uraia wetu (Fil 3,20).
Baba Mtakatifu  anasema,wakati huo sisi kama wafuasi wa Emmau tunalikwa kutazama mahali ambapo hakuna machweo, mahali ambapo upendo hautakuwa na kikomo, mahali ambapo tutapokelewa mmoja na mwingine kama zawadi ya Bwana kwasababu ya kutakiana mema na upendo, hurumana vilevile ma kushiriki uchungu na wale ambao wanateseka tukifikiria kuwa uchungu na majanga yao ni yetu pia.

Baba Mtakatifu Francisko anatoa  wito huo kuwa usikilizwe kwa unyenyekevu katika tafakari za siku hizi za kwenye mkutano wao ili waweze kukua daima na mawazo ya kindugu, kukomaa kwa dhati katika kukaribisha kwa moyo kwa maana wote ni mahuji kuelekea katika ufalme. Pamoja na hayo ni kusukumwa na hatua hizo kwa ujasiri na dhati  kuelelea katika umoja wa kweli. Mwisho amwabariki na kuwatakia  mema katika mkutano huo wakiongozwa na mapaji ya Roho Mtakatifu na kuwaomba sala zao kwa ajili yake.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.