Kama Mama Theresa , tufungue upeo wa furaha na matumaini kwa watu wengi walio kata tamaa na wenye kuhitaji kuguswa na huruma ya Mungu. Ni maneno ya Baba Mtakatifu Francisko aliyotolewa tarehe 5 Septemba 2017 katika Tweet ya Pontifex kwenye lugha 9. Ni siku ambayo inakumbuka miaka 20 tangu kifo cha Mama wa Maskini wakati huo, tarehe 4 Septemba ilikuwa ni kumbukumbu ya mwaka wa kwanza tangu kutangazwa kuwa mkakatifu na Papa Francisko katika viwanja vya Kanisa kuu la Mtakatitu Petro. Mama Theresa ni mwanzilishi wa Shirika la Wamissionari wa Upendo na mwenye tuzo ya amani ya Nobel ya mwaka 1979. Ni mtawa ambaye ni mfano wa pekee katika maajabu ambayo yanaweza kujikamilisha ndani ya kujitoa kwake Yesu Kristo.
Tarehe 26 Oktoba 1985 akiwa katika Baraza kuu la Umoja wa Mataifa, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa wakati huo Pérez de Cuéllar alimwelezea mama Theresa kuwa ni mwanamke mwenye nguvu zaidi katika dunia. Licha ya Mtawa huyo mdogo katika mavazi yake rahisi, alipendelea kujiita kuwa yeye ni kalamu ndogo ya risasi katika mikono ya Mungu. Karamu ndogo ya risasi lakini yenye uwezo wa kuandika kurasa nyingi kuhusu huruma na ambaye kwa nguvu ya imani yake aliweza kufungua nyumba nyingi za wahitahi hata katika maeneo yasiyoelezeka, kuanzia Quba hadi katika muungano wa nchi za Kisovietiki. Na kila mmoja aliyeuliza siri yake ni ipi alijibu kwa urahisi kwamba anasali.
Katika tukio la kutangazwa mtakatifu tarehe 4 Septemba 2016, hata Baba Mtakatifu alisema, tutakuwa na shida kidogo ya kumwita Mtakatifu Theresa, kwa sababu utakatifu wake uko karibu sana na sisi kiasi cha kuona kwamba yeye ni mwema na amekwishatoa matunda na hivyo kwa urahsi tutendelea kusema Mama Theresa. Aidha aliongeza; mtu huyo asiyechoka katika jitihada za huruma , atusaidie kuelewa zaidi na zaidi kwamba kigezo kimoja tu cha matendo ni upendo wa bure, bila kuwa na itikadi yoyote na dhamana yoyote, kutokuwa na ubaguzi na bila utofauti wa lugha , utamaduni, rangi au dini. Na kwamba Mama Theresa alipenda kusema hata kama sizungumzi lugha yao, lakini ninaweza kutabasamu.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |