2017-08-18 13:19:00

Mageuzi ya Mawasiliano katika kubuni mbinu mpya ya kiteknolojia


Mawasiliano katika mtazamo wa Baba Mtakatifu Francisko, ndiyo ilikuwa kichwa cha hotuba ya Mosinyo Dario Vigano Rais wa Sekretarieti ya Mawasiliano Vatican (SpC) wakati wa kufungua Mkutano wa 10 wa Mawasiliano ulio andaliwa na Baraza la Maaskofu nchini Brazili. Mkutano huo umefunguliwa tarehe 16 Agosti na utamalizika 20 Agosti.Mbele ya umati mkubwa wa waandishi wa habari na wahudumu wa mawasiliano huko Jimbo la Joinville Mkoa wa Mtakatifu Catarina Brazil; ametoa hotuba yake, ikiwa imegawanyika katika sehemu mbili, ambapo sehemu ya kwanza ikioonesha juu ya mawasiliano ya Baba Mtakatifu Francisko. Amesema kwamba kabla ya kujikita kwa kina juu ya mageuzi, ni lazima kutambua mtazamo wa hali ya halisi ya  mawasiliano ya Baba Mtakatifu Francisko, ni mawasiliano ambayo yaweza kuelezwa kuwa kwa namna ya kisayansi. Na zaidi amesema, katika matukio mengine anapenda kusisitiza ni jinsi gani Baba Mtakatifu Francisko alivyo na uweza wa kuunda misemo ambayo ni kama  aina ya mawasiliano, kwa kutumia ubunifu na urahisi usio wa kawaida, au kwa kutumia mifano na mafumbo.

Monsinyo Vigano’ amekazia kwamba, hiyo ni namna yake ya kuwasiliana na kila mmoja,ili kupunguza pengo kubwa linaloweza kujitokeza kuwezesha mwendelezo wake wa mazungumzo wakati wa kuwasiliana
Aidha amesema ni kwa njia ya maelezo na yenye kuwa na  huruma ambavyo ni msingi mkubwa wa  Baba Mtakatifu wakati wa mawasiliano yake. Mawasiliano hayo siyo kwamba yanatoka nje tu badala yake ni nyenye thamani ya kukuza uwepo wake na mahitaji wa wasikilizaji wake pia. Lugha anayo tumia Baba Mtakatifu Francisko  haisimami kamwe na wala kuwa nzito au kuchosha msikilizaji zaidi ina uwezo daima wa kuvutia na kuisikiliza sauti yake. Ametoa mfano kuwa, tendo la kusikiliza kwa kawaida ni jambo gumu na changamoto kwani mara nyingi linakutaka  uwe na uhusiano na wengine katika kuwasiliana.

Katika sehemu yake ya pili ya hotuba, Monsinyo Vigano’ amelezeza kwa kirefu na kushirikisha mchakato wa mageuzi ya Habari Vatican. Ameelezea mwanzo na maendeleo ya mageuzi ya Mawasiliano hayo  ya kwamba  yana mzizi mkuu unaotoka mbali na  zaidi sasa kwasababu ya ulazima na dharura ambayo tayari ilianzia katika Jubileo ya mwaka 2000. Mageuzi  hayo yameendelea, hadi kufikia hatua ya kiteknolojia ya digitali ambayo yamebadili namna ya utendaji kwa kila aina ya maisha yetu ya kila siku, ya kijamii, kisiasa na dini.
Halikadhalika amesema,mageuzi siyo kitu rahisi kama uchoraji kwa kukumbusha maneno ya Baba Mtakatifu Francisko aliyoyasema wakati wa Mkutano wao wa mwaka wa Sekretarieti ya Mawasiliano kuwa; Mageuzi siyo kupaka rangi vitu kidogo, bali mageuzi ni kutoa mfano muundo mwingine wa  vitu, kuvipanga kwa namna nyingine. Hii ina maana, siyo kwamba ni utaratibu rahisi tu , lakini pia ni namna ya kujua  kubuni mbinu ya kweli na mikakati ya utoaji wa mawasiliano ya Vatican.


Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.