2017-08-16 09:20:00

Maaskofu nchini Pakistani watoa wito kwa viongozi wa kisiasa kuepuka chochezi


Tume ya Kitaifa ya Haki na amani ya Baraza la Maaskofu Katoliki wa Pakistani wametoa wito kwa viongozi wa vyama vya kisiasa kuonesha ukomavu wa kisiasa na kuepuka chochezi. Wametamka hayo mara baada ya kuondolewa kwa Waziri Mkuu  Nawaz Sharif kutokana na uchunguzi wa kuhusishwa na rushwa. Maaskofu hao wanao wasiwasi mkubwa juu ya kuongezeka kwa vurugu ambazo zinaathiri wanachi na siyo tu wakristo.
Taarifa inakumbusha kuwa matukio ya kisiasa ambayo makahama Kuu imemwondoa Sharif tarehe 28 Julai 2017, inazidi kuleta mvutano na vurugu kubwa nchini humo. Kwani inasemekana watu zaidi ya Ishirini wamejeruhiwa kutokana na mlipuko wa bomu lililokuwa limetegwa ndani ya Lori la kubeba matunda tarehe 7 Agosti 2017 huko Lahore. Wakati huo hivi karibuni katika mji huohuo watu ishirini na sita wakiwemo Wakristo watatu waliuwawa katika shambulio la kujitoa muhanga.

Hata Kiongozi wa kundi la madhehebu kwa ajili ya amani kiitwacho Rawadari Tehreek ameonesha wasiwasi kuhusu  kuongezeka kwa mivutano hiyo ya kisiasa, anasema  kutumia vibaya utamaduni utaongeza moto zaidi katika jamii ambayo imechoka kuvumilia migogoro hiyo. Aidha ameongeza, ipo ofu ya kumwaga damu tena katika mwelekeo wa uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika mwaka kesho. Kwa njia hiyo Kiongozi huyo Samson Salamat ambaye ni Rais wa Madhebu ya Kikristo amewaalika kupiga marufuku ya  kufanya mijadala ya chuki. Ikumbuke kwamba Katika nchi ya Pakistani Bwana Sharif alikuwa ni waziri Mkuu  wa kumi na tano katika nchi ya Pakistani ambaye hakuweza kukamilisha mkataba wa katiba ya  uongozi kwa miaka mitano.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.