2017-08-09 15:32:00

Fatima:Hija katika madhabahu ya Mama Maria nchini Ureno mwezi huu


Askofu Mkuu Rino Fisichella Rais wa Baraza la Kipapa la Ushauri na Ujilishaji mpya  atakaye ongoza hija   ya mwezi huu  huko Fatima nchini Ureno. Tukio la hija hiyo  hilo linategemewa kufanyika Jumamosi  ya tarehe 12 na Jumapili ya tarehe 13 Agosti 2017 itakayo ongozwa na Kauli mbiu “Mtakatifu Maria Mama wa Mungu”. Nia ni kutaka kukumbuka tukio la  Mama Maria kuwatokea  watoto watatu  wachungaji  Francisko, Jasintha na Lucia.
Ikumbukwe kwamba hija  inaaangukia ndani ya  Wiki ya Kitaifa ya Wahamiaji, kwa njia hiyo  ni kama hija ya wahamiaja na wakimbizi. Tukio wiki ya wahamiaji  limefikia mwaka wa 45  nchini Ureno ambalo limeandaliwa Utume Katoliki kwa  ajili ya wahamiaji. Ni sehemu ya Kamati ya Baraza la Maaskofu ya kichungaji jamii na maendeleo ya binadamu nchini Ureno. Kauli mbiu ya mwaka huu ni kupokea   wakati ujao,kwa vizazi vijavyo vya wahamiaji ambao ni binadamu wa kesho.

Katika ratiba inayohusiana na hija katika Madhabahu ya Fatima, wataunganika siku ya Jumamosi 12 Agosti 2017  saa kumi na mbili na nusu za jioni , mara baada ya mkutano na vyombo vya habari kuwakilisha tukio. Saa tatu na nusu za usiku katika Kanisa dogo la kutokea Mama Maria,kutakuwa na baraka ya mishumaa na kusali Rosai . Saa nne na nusu usiku itafuatia misa ya kimataifa. Na baada ya misa hiyo itafuatia mkesha wa wa sala na kuabudi Ekaristi Takatifu. Jumapili tarehe 13 Agosti 2017 katika maporokia yote  na Jumuiya za kikristo nchini Ureno itakuwa ni siku ya mshikamano.

Sr Angela Rwezaula.
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.