2017-05-02 15:33:00

Papa: Mtakatifu Stefano ni shahidi wa utii na mfano wa Yesu!


Bwana ilainishe mioyo migumu, ambayo uhukumu kila kitu kilicho kinyume na sheria. Hayo ni maombi ya Baba Mtakatifu Francisko katika Misa ya asubuhi Jumanne tarehe 2 Mei 2017 katika Kikanisa cha Mtakatifu Martha mjini Vatican. Hawatambui ya kwamba huruma ya  Mungu ina uwezo wa kugezua mioyo migumu kama mawe na kuwa ya nyama. Mtakatifu Stefano ni shahidi wa utii, kama Yesu na ndiyo maana aliteswa. Baba Mtakatifu akitafakari somo la siku juu ya kifodini cha Mtakatifu Stefano, anasema, mkristo  ni shahidi wa utii. Waliomtupia  mawe Stefano hawakuwa na utambuzi wa Neno la Mungu, na ndiyo maana Mtakatifu Stefano aliwaita wenye shingo ngumu , wasio tahiriwa katika mioyo na katika masikio . Baba Mtakatifu anafafanua, mtu ambaye hakutahiriwa kwa nykati hizo ilikuwa sawasawa na mpagani.

Kwa njia hiyo Baba Mtakatifu anaomba  kutafakari namna ya kuwa na utambuzi wa Neno la Mungu katika Injili ya siku. Anasema  Kwa mfano wa Yesu aliwaita mitume wa Emau wapumbavu , hayo ni maelezo yasiyo toa sifa  japokuwa hayana nguvu kama yale aliyotumia Stefano.
Mitume wa Emau hawakujua, kwasababu walikuwa na  hofu, hiyo ni kwasababu hawakutaka kujiingiza katika matatizo, ilikuwa ni hofu tu japokuwa wao walikuwa ni wema na wako wazi katika ukweli. Wakati Yesu anawakaripia akifafanua maandiko matakatifu waliacha maneno yake yaingie  ndani yao na mioyo yao ikawaka tofauti na na wale walio mtupia mawe Stefano , walikuwa na hasira kuu, hawakutaka kusikiliza. Baba Mtakatifu anasema hili ni janga la kufunga mioyo na kuwa migumu. 

Zaburi ya 94 inawashauri  watu wake  wasifanye mioyo yao kuwa migumu. Hata Nabii Ezekieli anafanya ahadi nzuri ile ya kubadili mioyo  migumu kama mawe kuwa nyama, maana yake moyo wenye uwezo wa kusikiliza na kupokea ushuhuda wa utii. Mioyo migumu kama mawe   inafanya Kanisa liteseka sana Baba Mtakatifu anasema hayo kwa uchungu,mioyo ambayo haitaki kufunguka  na wala kusikiliza. Mioyo ambayo siyo kwa kutambua tu lugha ya kuhukumu bali inatambua kuhumu hasa, haiwezi kusema, bali inauliza kwanini unasema hivi, kwanini hiki, nieleze…ni mioyo iliyofungwa , wanajifanya kuelewa kila kitu na kwamba hawana haja ya kuelezea.

Kitendo cha Yesu kuwakaripia waliowaua manabii , ilitokana na kwamba  waliwaelezea  mambo ambayo  hakuwa wanapenda . Hayo yote ni kwasababu moyo ulio fungwa hatuoi  nafasi ya roho mtakatifu aingie. Hapakuwapo na nafasi ya Roho Mtakatifu katika mioyo yao. Lakini katika somo linaeleza kwamba Mtakatifu Sefano  akiwa amejaa Roho Mtakatifu alikuwa ametambaua yote. Yeye alikuwa ni shuhuda wa utii wa Mungu ambaye ni Neno aliyefanyika mwili. Kwa njia hiyo, moyo uliofungwa, mgumu , moyo wa kipagani hawezi kuacha nafasi ya Roho mtakatifu aingie kwa sababu ya kujitosheleza.

Baba Mtakatifu Francisko anasema mitume wawili wa Emau ndiyo sisi, pamoja na wasiwasi , dhambi ambazo mara nyingi tunatamani kwenda mbali na masalaba , na majaribu. Ni bora kuacha nafasi , ili mioyo hiyo iwashwe na Yesu mwenyewe.
Aidha Baba Mtakatifu Francisko amelezea juu ya watu wale ambao walikuwa wagumuna mioyo yao imefungwa kwa kushiria sheria, na hawakutaka kusikiliza Yesu… wao walikuwa wanaongea mambo mabaya zaidi ya yale yaliyo tamkwa na Mtakatifu Stefano. Baba Mtakatifu anaoanisha kitendo cha mawe na mfano wa mwanamke mzinzi, kwamba kila mmoja aweze kuingia katika mazungumzo kati ya moyo mgumu na Yesu, ambapo moyo mguni ni kama wa yule mwathirika mwanamkwa ambaye Yesu aliwajibu wale waliokuwa wakitaka kumtupia mawe ya kwamba watazame ndani ya mioyo yao.

Kwa kumalizia Baba Mtakatifu amesema ni kutazama huruma ya Yesu, Shahidi wa uti, ambaye ni shahidi mkubwa aliye toa maisha kwa kutufanya tuonje huruma ya Mungu sisi wenye dhambi na wadhaifu. Pia tuweze kuingia katika mazungumzo na kuomba neema ya  Bwana alainishe kidogo mioyo yetu migumu, hata kwa wale wenye mioyo iliyofungwa daima katika kushikiria sheria wakihukumu kila kitu kitu kilicho kinyume na sheria yao. Kwasababu hao hawajuhi kwamba Neno alifanyika  mwili na kwamba Neno ni shahidi wa utiii. Hawajui kwamba huruma ya  Mungu inao uwezo wa kubadilisha mioyo migumu kama mawe na  kuwa mioyo ya nyama.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.