2017-04-05 16:48:00

Tunayo kazi ya kusikiliza kwanza bila kuwa na haraka ya kujibu


Asubuhi ya tarehe 5 Aprili 2017 Baba Mtakatifu Francisko kabla ya katekesi amekutana na kuzungumza na wawakilishi wa Viongozi wa Kiislam kutoka Uingereza katika Ukumbi mdogo wa Mwenyeheri Paulo VI mnji Vatican.
Viongozi hao wako Roma katika tukio la Mkutano kuhusu  kushirikishana, elimu na kutuma nguvu. Aliye waongoza no Askofu wa Westminster , Kardinali Vincent Nichols,ambaye ametoa salam baada ya utangulizi wa Kardinali Jean - Louis Tauran, Rais wa Baraza la Kipapa wa mazungumzo ya kidini.
Kardinali Nichols akiwa ameongozana na viongozi wanne kutoka Jumuiya ya Kiislam ya Ungereza,kama wawakilishi wa matawi yao ya  Sunni na Shia,Kardinali amesema wanafanya kazi kwa pamoja kwa ajili ya amani na mazungumzo ya kidini. Aidha kardinali amesema Papa ni mfano halisi wa kiongozi wa wote. Vilevile amemshukuru Baba Mtakatifu Francisko kwa ujumbe wake alio utoa mara baada ya shambulio la kigaidi , na kusema kwamba shambulio hilo kwa wakati huu linawakilisha changamoto kubwa, kutokana na hilo kwao ni fursa ya kutoa sauti ya pamoja kwa ajili ya muungano wa nchi , kwa ajili ya amani na imani kwa Mungu.

Na baada ya hotuba ya Kardinali, Baba Mtakatifu naye ametoa hotuba fupi kuhusiana na mkutano huo , akisema anayo furaha kwa ajili hiyo na pia mesisitiza juu ya kusikiliza , na hasa katika mazungumzo ya kidini , jambo kubwa na muhimu ni kusikiliza. Amebainisaha kuwa haiwezekani kufanya mazungumzo juu ya dini kama hakuna utambuzi wa imani binafsi. Mazungmzo ya kidini yana anzia daima na imani binafsi. 
Baadaye kuna changamoto za hapa na pale kwa mfano wa  asiye amini ninavyo amini au kuishi kama ninavyoishi na akaongeza hiyo siyo lazima awe adui, bali ni ndugu wa kutembea  njia nyingine na mwingine njia ya Mungu. Vile vile kuna changamoto ya ukosefu wa ukweli.

Mazungumzo ya kidini siyo mkakati , bali ni mazeozi ya dini ya binadamu mbele ya Mungu na mbele ya wenzake katika ubinadamu kwasababu sisi sote ni mahujaji kulekea ukweli.Kwa njia hiyo Baba mtakatifu Francisko amesema kwamba  anapenda kutafakari kazi muhimu inayo paswa kufanyika leo hii kati yetu binadamu na hasa kazi hiyo ni ya sikio, kwa maana ya kusikiliza bila kuwa na haraka ya kutoa jibu.Maana yake ni kupokea neno kutoka kwa ndugu kaka na dada ndipo  baadaye unafikiria  kutoa yako binafsi. Lakini uwezo wa kusikiliza ndiyo muhimu sana, Baba Mtakatifu ametoa mfano na kisema inapendeza kuona  watu wenye uwezo wa kusikiliza wengine, wanapokuwa wanaongea, hawatoi sauti kali. Wanaongea kwa sauti ya upole…tofauti na wale wasio kuwa na uwezo huo, kwani wanaongea kwa sauti kubwa na hata kupayuka.Ka njia hiyo kati yetu ndugu tunapaswa kuongea kwa taratibu na kwa utulivu,katika kusikiliza  ili kutafuta njia ya kutembea pamoja.Tunapotambua kusikiliza na kuongea tayari ndiyo njia tuliyomo.

Viongozi wa Kiislam walioshiriki mazungumzo na Baba Mtakatifu Francisko kutoka Uingereza walikuwa Rais wa Baraza la Kiislam Uingereza, Ali Raza RIZVI: Muhammad Shahid RAZA, mwenyekiti wa jukwa la waislam Uingereza ; Shaykh Ibrahim MOGRA, Msaidizi wa mwenyekiti wa Jukwaa Wakristo na waislam Uingereza; na Sayed Ali Abbas RAZAWI, Mkurugenzi Mkuu wa chama cha Scoltland cha  Ahlul Bayt .

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.