2017-03-26 12:55:00

Usihukumu kwamba wanastahili kifungo maana hatujui historia yao


Ziara ya Baba Mtakatifu katika Gereza la Mtakatifu Vottore ilikuwa ni moja ya ziara yenye msisimko wakati anaelekeza safari yake Milan. Amewashukuru kwa makaribisho yao na kusema anajisikia kuwa mmoja kati yao.Maneno hayo ameyatamka kwanza  kwa wafungwa  walio mpokea kwa shangwe kubwa na kuwasalimia kila mmoja kwa mkono na kuongea nao kwa maneno mepesi kabisa kabla ya kwenda kula chakula cha mchana ndani ya Magereza.
Mwandishi wa Radio Vatican, alipata habari zaidi kuhusiana na makaribisho ya Baba Mtakatifu   kutoka kwa Padre anayehudumia Kanisa dogo la magereza hiyo.Amesema umekuwa muda mzuri sana na wenye maana  kwasababu Baba Mtakatifu amefanya uchaguzi wa ajabu, yeye binafsi amewasalimia watu zaidi ya 850 wakiwemo hata maaskari.Yeye binafsi amewapitia na kutoa mkono wake, au akitoa neno lake wakati huo huo akipita kumetokea aina fulani ya kimya kana kwamba utafikiri ni sala ndani ya Kanisa, wakati yeye kwa mwendo taratibu anawasalimia.

Kuhusu uzoefu  na hisia za maneno ya Baba Mtakatifu  Padre anasema , Baba Mtakatifu Francisko amesema hawali ya yote hatupaswi kusema kwamba hawa wanastahili kwasababu kwamba sisi hatujuhi historia ya mtu fulani,au hutujuhi kilichopo nyuma yake.Yote hayo tunapaswa kumwachia Mungu aliye hakimu, tunachopaswa kufanya sisi ni kutazama dhambi zetu,na taabu zetu. Baadaye Baba Mtakatifu amegusia  juu ya Injili ya Mtakatifu Matayo  isemayo "ni wakati gani nilikuona gerezani, kwa namna hiyo akaongeza ;“ninyi kwangu ni Yesu”.Aidha Baba Mtakatifu Franciko amesema juu ya mitazamo yao,kwamba inapaswa kuona upeo wa mkubwa , kwasababu baadaya ya gereza kuna upeo mkubwa wa maisha na matumaini.

Baada ya makutano hayo Padre anasema, mmoja wa wafungwa wakati wanarudi , amemwambia kuwa, kwa masaa mawili yamepita utafikiri siyo mfungwa gerezani. Padre anasema kwa namna hiyo ni kama vile amewapatia uhuru wa ajabu katika makutano hayo.Wengi wao walikuwa na furaha kubwa hadi wengine kuoneshaa machozi .Kwa maana hiyo unaweza kufikiria kama kwamba Baba Mtakatifu amefungua milango ya gereza, kwasababu wote tulikuwa pale waume kwa wanawake mbele ya Baba ambaye ametoa matumaini na nguvu.

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.