2017-03-22 17:06:00

Baba Mtakatifu amepokea zawadi ya sweta 1000 kwa ajili ya wahitaji


Baba Mtakatifu Francisko amepokea zawadi ya sweta nyekundu na mifuko midogo zaidi ya 1,000 zilizotengezwa kwa ajili ya usafi binafsi kwa ajili ya wahitaji kutoka kwa wajasiriamali wa Baa za ufukweni.
Ni mpango ulio anzishwa kwa ajili ya kiangazi mwaka huu kwa mshikamano kwa ajili ya watoto na watu wenye kuwa na hali ngumu.
Zaidi ya wajasiriamali 1,500 wenye baa fukweni  kutoka nchini kote Italia  wakifuatana na familia na wafanyakazi wao walikuwepo katika viwanja vya Mtakatifu Petro kusikiliza katekesi ya Baba Mtakatifu Francisko.

Makutano hayo yaliandaliwa  na (S.I.B.) chama cha utetezi wa baa za baharini nchini Italia , pamoja na chama cha biashara (FIPE ) na kwa ushirikiano wa umoja wa wasafirishaji wa wagonjwa nchini Italia huko Lourdes na madhabahu ya kimataifa.(UNITALISI. 
Uwanja wa Mtakatifu Petro ulifurika kwa rangi nyekundu za masweta walikuwa wamevaa waamini kutokana na uwepo wao kwa mara ya kwanza Vatican.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.