Mtakatifu Yosefu awawezeshe vijana kuwa na uwezo wa kuota ndoto,wa kujiweka katika hatari katika kukabiliana na mazoezi magumu wanayo yaona katika ndoto zao.Haya ni matashi mema ya Baba Mtakatifu Francisko aliyoyatoa kwenye Kikanisa cha Mtakatifu Martha kilichoko mjini Vatican wakati wa misa ya asubuhi Jumatatu 20 Machi 2017 Baba Mtakatifu katika mahubiri yake, anaelezea sura ya Mtakatifu Yosefu msimamizi katika udhaifu na katika ndoto ya Mungu. Kanisa katoliki likiwa linafanya kumbukumbu yake badala ya tarehe 19 kutokana na kwamba ilikuwa tarehe 19 Machi 2017 iliangukia Jumapili ya tatu ya kwaresima.
Mtakatifu Yosefu alitii amri ya Malaika aliye mtokea katika ndoto na kumchukua
mchumba wake Maria akiwa na mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu kama Injili ya Mathayo
isemavyo.Ni mwanaume mkimya na anatii.Yosefu ni mwanaume anayebeba mabegani ahadi
ya uzao, ahadi ya urithi,ahada ya ubaba wa mtoto ambayo ilikuwa imeshatabiriwa na
kupangwa .Baba Mtakatifu Francikos anasema , mwanaume huyo ,mwotaji ana uwezo wa kukubali
zoezi hilo. Zoezi ambalo tayari linaweza kutufundisha jambo fulani kwetu sisi katika
kipindi cha nguvu kwa maana ya uyatima. Mwanaume huyo anachukua ahadi ya Mungu na
kuipeleka mbele kwa ukimya na kwa nguvu, anaipeleka mbele kwasababu ni ule utashi
wa Mungu anaotaka utimilizike.
Mtakatifu Yosefu ni mtu anayeweza kutueleza mambo mengi lakini haongei, ni mtu anaye
jificha, ni mtu mkimya , ambaye anayo madaraka makubwa kwa wakati huo, lakini hauoneshi.
Baba Mtakatifu Francisko anachambua kwamba mambo ambayo Mungu anamwaminisha katika
moyo wa Yosefu , ni mambo madhaifu ya ahadi ambayo ni ahadi ya dhaifu .Kam vile kuzaliwa
kwa mtoto, kukimbilia Misri,haya ni mambo ya hali ya udhaifu. Lakini Yosefu anayachukua
katika moyo wake na kuendelea mbele, mambo hayo madhaifu. Je ni namna gani ya kupeleka
mbele mambo madhaifu? Anasema ni kwa njia ya kubembeleza kama vile umchukuavyo mtoto
mdogo mikononi.
Ni mtu asiye ongea bali yeye anatii, ni mtu mwema ni mtu mwenye uwezo wa kuchukua
mbele ahadi kwasababu iweze kuwa imara na salama, ni mtu anaye hakikishia msimamo
wa Ufalme wa Mungu, ubaba wa Mungu , ni sehemu ya kuwa watoto wake kama vile mtoto
wa Mungu.
Baba Mtakatifu Francisko anasema kwamba, anataka kufikiria Yosefu kama kwamba ni msimamizi
wa wadhaifu , yaani udhaifu wetu pia kwani na pia nao uwezo wa kuzaa mambo mengi
mazuri kutoka katika katika yale madhaifu yetu, ambazo ni dhambi zetu. Yosefu ni msimamizi
wa udhaifu wetu ili imani yetu iweze kuwa imara. Yosefu ni mtu wenye uwezo wa kuota,
anachambua Baba Mtakatifu , na hivyo yeye ni msimamizi wa ndoto ya Mungu. Kwa maana
ndoto ya Mungu ni kuwakoa wote,na kukomboa ndiyo kazi aliyo kabidhiwa.Fundi Seremala
huyo ni mkubwa! Anasema Baba Mtakatifu Francisko, kwani katika ukimya, anafanya kazi,
analinda, na kuchua mbele udhaifu kwani anao uwezo wa kuota ndoto.Kwa njia hiyo ni
Yosefu ni sura yenye kutoa ujumbe kwa watu wote.
Anamaliza akisema, ni kumuomba Yosefu aweze kutupatia uwezo wa kuota kwasababu
tukiota mambo makubwa , mambo mema, tunakaribia ndoto ya Mungu ,kwa maana ndiyo ndoto
ya Mungu anayoota kwa ajili yetu.Na kwa ajili ya Vijana kama vile alivyo kuwa naye
kijana awawzeshe uwezo wa kuota kujihatarisha na kuchua wajibu wa mazoezi magumu
ambayo wameona katika ndoto zao.
Na kwa wote Mtakatifu Yosefu aweze kutusaidie tuwe waaminifu ambao tukuze mitindo
ya haki, kwasababu yeye alikuwa mwenye haki , na kuishi katika ukimya , kuwa na maneno
machache, kukua katika ukarimu na uwezo wa kutunza udhaifu wetu binafsi na hata wa
wengine.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahuli ya Radio vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |