2017-03-17 15:37:00

Wanglikani nchini Uingereza kutetea wanao nyanyaswa majumbani!


Jumuiya za kikristo zinapaswa kutambua kwamba maeneo ni salama ambapo waathirika wa unyanyasaji wa majumbani  wanapaswa kuchukuliwa kwa makini, kuaminiwa na kuheshimiwa . Na kwa wale walio husika na ukiukwaji wanapaswa kuchukuliwa hatua kwa kuoneshwa wazi matendo yao.Hiyo ndiyo ufupisho wa lengo la hati mpya ya Kanisa la Uingereza ambayo imerudia  upya kutazama jambo hilo , kwani ilikuwa tayari imechapishwa  mwaka 2006.
Mashambulizi na kusumbuliwa ndani ya nyumba , itakuwa ni moja ya mada katika semina na majadiliano ya kina , semina ya maandalizi na  mikutano ya makundi ya vijana.Wale wanao husika na kukabiliana na unyanyasaji wa majumbani ndani ya Kanisa la Uingereza wanalazimika pia kushirikiana na wawakilishi wa Serikali ya Uingereza inayojikita katika uwanja huu na pia sekta mbalimbali za vyama.

Mkutano wa Maaskofu wa Kianglikani ,katika waraka mpya wameomba kwamba wafanyakazi  na kujitolea ambao wanafanya kazi karibu na watoto, vijana na watu wazima wenye kuishi katika mazingira magumu , kufanya  mafunzo maalumu na maandalizi ambayo yatawawezesha kukabiliana kwa kina zaidi katika kutafuta haki ya wale wanao nyanyasika  majumbani , na kuwatambua wahusika pia kupata  kuwasaidia waathirika.
Waraka huo wa pili umetolewa na maaskofu  wa kianglikani nchini Uingereza wenye mada ya “kuhamasisha usalama zaidi wa Kanisa, unawaajibisha maaskofu mapadri, mashemasi, wasomaji neno la Mungu, walei na kila mtu binafsi anaye jibidisha katika hali hii ya Kanisa kuheshimu mwongozo wa kanuni  katika suala hili la manyanyaso ya majumbani.Askofu wa kuanglikan wa Bath na Well  Peter Hancock, kwa miaka mingi yuko mstari wa mbele katika kulinda waathirika anasema , Kanisa la Uingereza linajibidisha  kusimamia wale walio athirika na wale na mbao kwa sasa wakao katika mchakato huo.
Askofu anakumbusha kwamba manyanyaso ya kila aina ni kinyume na mapenzi ya Mungu na ni ukiukwaji wa utu wa mwanadamu.Kila mmoja napaswa kuwa sehemu ya kuzuia au kusimamisha matukio hayo, pia Kanisa la Uingereza linaonesha wajibu wake kwa nguvu kusimamia kila aina ya manyanyaso.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.