2017-03-16 14:25:00

Diplomasia ya majadiliano na watu kukutana ni kipaumbele cha Papa


Hivi karibuni Askofu mkuu Bernadito Auza mwakilishi wa kudumu wa Vatican kwenye Umoja wa Mataifa alitoa hotuba katika ukumbi wa Seton wa Chuo Kikuu huko New Jersey Marekani kuhusu diplomasia ya Baba Mtakatifu Francisko,na amefurahishwa kuona anawahutubia ikiwa kama mojawapo ya matendo ya Juma la kwanza la  kwaresima katika Ukumbi huo wa Chuo Kikuu na kumushukuru Profesa Bartoli kwa kumpatia  fursa hii kuzungumzia na wanajumuiya ya Seton kuhusu Diplomasia ya Baba Mtakatifu Francisko, mada ambayo anasema huenda ikawa sawa katika  moyo wa utambulisho Katoliki katika Ukumbi wa Seton.Katika historia ya Kanisa,anasema,  hatuzungumzi historia ya  kuvunjika au kuanza upya,ni kuongea mwendelezo unao wezekana wa  safari ya umilele inayoongozwa na mafundisho ya kudumu kwa mantiki ya mazingira ya dunia inayobadilika.Anapenda kutoa mfano wa mashua thabiti ya Mtakatifu Petro kwamba, japokuwa inaonekana kuelea huku ikiyumbishwa na  mawimbi makali.Hiyo ndiyo njia anayopenda kufikiria kuhusu  diplomasia ya Vatican, kati ya Baba Mtakatifu Francisco na watangulizi wake,kwasababu hakuna mpasuko bali mwendelezo.

Diplomasia ya Vatican ni utume wa  kazi ya kutenda katika dunia iliyomezwa na malimwengu, Kanisa na kwa jina  la Kanisa.Kama Kanuni na utume wake inatenda chini  ya misingi na Kanuni  zake "wokovu wa roho ndiyo sheria kuu ya Kanisa.Inawezekana  kutimiza kanuni  hiyo tu kama inatambua jinsi ya kunyambulisha ishara za nyakati na kuzitafsiri katika mwanga wa Kristo,  namna ya utambuzi huo  na kutenda ipasavyo". (mwanga wa mataifa 4).
Ana amini kwamba ni kweli hasa katika mazingira ya uwepo wa Vatican katika Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya kimataifa. Lengo kuu kwa ujumla la uwepo wa mwakilishi wa kudumu wa Vatican katika  umoja wa Mataifa ,daima umekuwa  ni kuleta chachu ya Injili na Kanisa kwenye milenia nyingi  ya uzoefu wa binadamu na ukweli katika utata wa mahusiano ya kimataifa na katika mijadalaya kimataifa kuhusu matatizo yayo ikabili dunia yetu.

Wengi wanauliza kwanini Vatican inataka kuwapo katika umoja wa mataifa.Je sasa siyo mojawapo ya Umoja wa mataifa ,kama Rais mmoja hivi karibuni amesema ni kama  club kwa ajili ya kuwa pamoja kuongea na kuwa na muda mzuri. Alihitimisha akisema hii ni  mbaya sana.!
Lakini Askofu Mkuu Auza anasema, anaamini kwamba kuwa pamoja na kuzungumza na kuwa na wakati mzuri , siyo jambo la kusikitishana wala baya sana , bali katika Umoja wa Mataifa hakuna huzuni akitoa mfano wa mfululizo wa  mashairi   ya kale ya wimbo wa Dan Fogelberg  ukisema “ hatuna isemayo “zaidi ya hapo tumekuwa samaki katika bahari,” na “tumekuwa nyota ya juu katika mbingu” , na “mbaya kama wao hawana nguvu zaidi kuliko mlima mkuu “,na “mbaya zaidi bado kama wao siyo” ,”ni kweli zaidi ya mti wowote uliowahi kukua,” kuingia ndani kuliko msitu unao anza kuota”.(Taz “Longer  na Dan Forgelberg).

Hata hivyo, kwa nini, kweli, Vatican inashiriki kikamilifu sasa katika Umoja wa Mataifa?.Umoja wa Mataifa, kama mnavyojua vizuri, ulizaliwa kwenye masalia ya Vita Kuu ya Pili ya dunia mwaka 1945. Nchi 51 wanachama walisaini Mkataba wa Umoja wa Mataifa huko San Francisco mwaka1945.
Lakini hakika Vatican haikuwa hakika upendeleo kwa mara kwanza .Mara baada ya kuanzishwa Umoja wa Mtaifa , Vatican kwa kiasi fulani ilikuwa na tahadhali kuhusu hilo.Ilitambua haja ya haraka kwa ajili ya mashirika ya kimataifa ya kwamba wangeweza kufanikiwa katika shirikikisho la Mataifa,lakini ilikuwa bado na wasiwasi kadhaa .Wasiwasi ulikuwa kwamba Mkataba wa Umoja wa Mataifa, huku wakitambua usawa wa nchi, hawakutoa  kanuni hii, tangu wanachama 5 wa kudumu wa Baraza la Usalama,jambo jingine ni kwamba siyo wanachama wote walishiriki wa nchi nyingine kwa mfano hasa nchi zile ndogo zilizokuwa zimepata uhuru dhidi ya wakoloni,nchi hizo zilikuwa zimetengwa.Suala jingine ni kwamba walijadili matatizo lakini hayakuweza kutatuliwa hadi kufikia mwaka 1953, Papa Pius XII aliuliza hadharani: "Je, katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limeundwa kwa ajili ya kuweka Mikataba tu na  kwamba kamwe hawezi kuweka katika vitendo?.

Ingawa Vatican haikuwa mojawapo ya sehemu ya Umoja wa Mataifa kwa  siku za mwanzo, mara nyingi walishiriki katika kazi rasmi na isiyo rasmi ya Umoja wa Mataifa lakini kwa kupewa mwaliko. Hatima Aprili 1964 Vatican ikawa na mwakilishi wa kudumu wa  kwenye Umoja wa Mataifa na kuanza utume wake huko New York.Hii ilikuwa inafaa na siyo kwasababu ya kujihusisha kwa haraka Vatican katika maamuzi ya Umoja wa Mataifa , bali zaidi ya yote ni kwasababu ya nguzo ya nne ya Umoja wa mataifa ilivyowekwa katika Mkataba wake na kujieleza vizuri sana ,kwani ni nguzo nne kuu ya mafundisho katoliki ya kijamii  isemayo kuzuia vita na kuhamasisha amani, ulinzi na nafasi ya utu wa mwanadamu na haki; maendeleo ya binadamu;na kusaidia mataifa katika kutoa kutoa maoni yao na kuheshimu mikataba ya kimataifa na sheria.Katika kipindi cha miaka 53 ya uwepo wa Vatican katika Umoja wa Mataifa huko New York,mara tano mapapa wamefanya ziara katika ofisi za  Umoja wa Mataifa; Mwenye Heri Paulo VI  Oktoba 1965, MtakatifuYohane Paulo  II mwaka 1979 na 1995, Papa Benedikto XVI mwaka 2008, na Papa Francis 2015. katika ziara hizi, mapapa walionyesha heshima kwa taasisi hiyo ambayo wanaichukulia  kuma chombo muhimu kwa ajili ya dunia.Kila Baba Mtakatifu aliyefika katika ofisi hiyo aliweza kutoa hotuba na kuacha ujumbe muhimu kwa ajili ya tafakari binafsi na hata kwa ngazi ya kimataifa kwa pamoja.

Askofu Mkuu Auza anandelea, hadi hapo ameendelea kuelezea juu ya diplomasia ya Vatican katika ngazi ya kimataifa na hasa katika Umoja wa Mataifa Katika ngazi ya nchi na nchi, leo hii Vatican ina uhusiano wa kidiplomasia na nchi 182 kati ya 193 katika dunia na nyingine ziko katika orodha ya maandalizi. Wapo mabalozi wa kitume 116 wa kudumu katika utume duniani kote wanao wakilisha Vatican katika mtandao wa kina kidiplomasia. Na kama tunavyofikiria  maaskofu wetu, na makleri , watawa wanaume na wanawake , makatekista na walei anatoa mfano akiwaeleza wanafunzi kwamba ni sawa vitengo vya ujasusi nchini Marekani au pia vya nchini Urusi kwani  hakuna mtu awezaye kupambana nasi katika ukusanyaji wa taarifa na shughuli kwa ngazi ya chini.Askofu Mkuu Auza anatoa mfano halisi wa historia binafsi juu ya kupata habari hizo kutoka sehemu ambazo siyo rahisi kuzipata, akisema kwa upande wa Kanisa ni rahisi kwasababu ya uwepo wa wamisionari wengi katika kila kona ya  maeneo ya dunia ambayo kwa mtazamo rahisi siyo vyepesi kupata habari hizo. Kutokana na vikwazo vya muda, ni lazima sasa kuanza sehemu ya pili ya majadiliano, yaani, vipaumbele vya dipolmasia ya Baba Mtakatifu Francisko kwamba,katika utumishi wake lazima kutenda kwa kina zaidi.

Kabla ya  kutaja masuala maalum ambayo wao wanapaswa kuyatekeleza katika nchi moja na katika ngazi ya kimataifa ,anaonesha hawali ya yote dhana ya kukutana na mazungumzo.Ni tunu na dhahabu inayofunga mahusiano pamoja na meneno na matendo ya Baba Mtakatifu.Ule msukumu una maana kuu siyo tu  kwa ajili ya shughuli za kichungaji na kiroho kwa Kanisa, bali hata juu ya masuala ya kiuchumi, kijamii na kisiasa kwa nyakati zetu.
Baba Mtakatifu Francisko anasisitiza juu ya masuala ya "utamaduni wa kukutana , mshikamano na upendo". Kila asemapo kuhusu masuala ya kijamii na kuhusu maswali pamoja na athari kubwa ya kisiasa, yeye daima anathibitisha diplomasia ya kukutana kuongoza ili kuelekea maarifa bora ya kuheshimu na kuheshimiana. Ni diplomasia ya mazungumzo katika  kutatua migogoro, kuhamasisha  umoja na kupambana  na tabia za kubagua. Ndiyo inaitwa safari ya pamoja ni kama njia ya maisha. Hii ndiyo diplomasia kwamba fursa zaidi na  heshima kwa nchi zilizo dhaifu, Kanuni na  sheria juu ya sheria ya nguvu, uaminifu  na mahusiano mazuri miongoni mwa mataifa na watu zaidi ya tuhuma kwa pande zote. utamaduni wa kukutana hauwezi kupatikana kwa kujenga kuta na kukuza upweke, bali ni  kwa njia ya madaraja na milango wazi.

Askofu Mkuu Auza anawaeleza wanafunzi jinsi isivyo  rahisi kueleza tafakari zote za Baba Mtakatifu Francisko kwasababu ya kutokutaka kuwaibia muda wao wa utafiti na wa kufanya kazi katika majumba yao ,lakini masuala ambayo Baba Mtakatifu anapendekeza  kwa diplomasia ya mazungumzo, ujenzi wa madaraja na kukutana ni masuala ya kijamii pamoja na athari za nguvu ya kisiasa. Watu wanauliza,kwa nini Kanisa, kwa nini Baba Mtakatifu anajali kuhusu masuala yenye utata ya kijamii na kisiasa? jibu fupi kwa sababu Yesu anajali! na kama Yesu anajali, Baba Mtakatifu  na Kanisa hawawezi kutokujali pia.Aidha anasema ,wengi wenu mnajua   moyo wa sherehe za ufunguzi wa kifungu cha Mtaguso wa  Vaticani wa Pili   kuhusu masuala ya kichungaji kwa  Kanisa katika waraka wa “Kanisa katika Ulimwengu Mamboleo”  (Gaudium et Spes): "furaha na matumaini, masikitiko na shughuli za watu wakati huu, hasa wale ambao ni masikini au kwa njia yoyote wanateswa ndiyo  furaha na matumaini, masikitiko na shughuli za wafuasi wa Kristo. Hakika, hakuna kitu cha dhati  ya binadamu kushindwa kuongeza sauti  katika nyoyo zao.

"Kwa njia hiyo Kutokana na maneno na matendo juu ya maswali makubwa na changamoto zinazotukabili dunia ya leo , Baba Mtakatifu Francisko anatualika kufanya hivyo ili sisi wenyewe tupate kujivika furaha na huzuni wa dunia hii, ili tupate kuchafua  mikono yetu, kuwa na harufu ya kondoo , kwa kutoa huduma katika mahospitali, kujihusisha katika kukuza na kutekeleza diplomasia ya mazungumzo na kukutana,Hii ndiyo roho  inayo hamasisha Vatican kuwapo katika  Umoja wa Mataifa na katika mahusiano baina nchi zote duniani.Inatembea kimya bila kusema lolota wakati huo huo ikitoa ushuhuda wa pekee wa Vatican na Kanisa katika umahiri,kwani kuna haja ya kuepuka kujitambulisha kwa njia yoyote  kisiasa au kiitikadii na hivyo kulinda utambulisho wetu wa kipekee na ushawishi Kitaifa.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.