Miongoni mwa mipango mingi iliyofanyika kuienzi Siku ya Wanawake Duniani iliyofikia kilele chake tarehe 8 Machi 2017 ,Utume wa Kanisa Katoliki huko Brisbane nchini Australia uliandaa tukio la kwa ajili ya wahudumu wake ambapo waliwasilisha historia za wawake wamissionari kwa huduma zao za ajabu katika jumuiya na kwa ajili ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu na hatarishi; watoto yatima na wale wote wanaohitaji msaada wa pekee. Baadhi ya historia hizi zilitangazwa hata katika vyombo habari na mitandao ya kijamii kwa njia ya utume Katoliki nchini Australia kwa kuweka mfululizo wa matukio mbalimbali waliyo yaita “wanawake na utume”.
Mfululizo wa matukio hayo ulitolewa wiki iliyopita ukiwa unawakilisha mada ya Siku
ya wanawake duniani kwa mwaka 2017, kwa kauli mbiu “uwe pembeni kubadilika.Wanawake
wa utume wanatoa historia za watawa na wanawake walei kama viongozi katika utume
wakishiriki kwenye elimu , afya , huduma za jamii na malezi ya kiroho katika jamii
ya bara la Asia, Afrika, Amerika ya Kusini na Australia.
Naye Padre Brian Lucas , Mkurugenzi wa Taifa wa Utume Katoliki Australia anasema karibu
sehemu zote ambapo kuna Kanisa , wapo wanawake wenye ari, ambao wako mstari wa mbele
na wengine hawaonekani , hawa siyo kwamba ni atawa tu bali wapo hata mamilioni ya
wanawake walei wanao jitoa na wenye utajiri mkubwa wa imani.Anaongeza, “mfululizo
wa picha na video ni kuonesha dhamira kubwa kwa kutoa ufahamu kwa nini wanahamasisha
wanawake hawa wa ajabu katika upendo huruma , na msamaha wao kwa sasa ili kutuhamasisha
hata sisi” .
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kswahili ya Radio vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |