Mazungumzo ni njia mwalimu : amani inapatikana kwa njia ya mazungumzo, na siyo
kwa nguvu : ni maneno kwa ufupi yaliyomo katika ujumbe wa Kardinali Philippe Ouédraogo
Askofu Mkuu wa Ouagadougou nchini Burkina Faso alio utuma katika Jukwaa la Kimataifa
ambalo limefanyika kuanzia tarehe 3 hadi 7 Machi 2017 lenye kuwa na mada ya “mazungumzo
ya kidini kwa ajili ya kuelemisha amani”.
Tukio hilo limeandaliwa kutokana na mwendelezo wa Jukwaa la kimataifa la tarehe 29
Mei 2015, likiwa na mada ya “elimu ya amani na maendeleo kwa njia ya mazungumzo ya
kidini na utamadunisho”. Jukwaa hilo lilifanyika huko Cotonue nchini Bennin, kwa
upendeleo wa Albert Tévoedjeré,mjumbe maalum wa Umoja wa uchumi na fedha Afrika
Magharibi (UEMOA.) Wakati wa hotuba yake huko Ouagadougou Tévoedjeré , anathibitisha
kuwa ili dini iweze kupinga chuki,kwanza inahitaji kujifunza kusali kwa pamoja na
kufanya kazi kwa pamoja ili kupunguza hali ya umasikini na hivyo, lazima Afrika iachane
na maeno tu bali kuweka kwenye vitendo malengo ya dhati kwa ajili ya maendeleo ya
Bara kwasababukwa kuishi pamoja, uwezekano hupo wa maendeleo endelevu ya Afrika.
Naye Michaëlle Jean, Katibu Mkuu wa Mashirika ya Kimataifa wa Afrika ya Magharibi(OIF),anasema
;utofauti wa tamaduni , na dini unajieleza kwa amani juu ya misingi ya umoja wa uzalendo
na kijamii kwa urithi wa miongo hadi miongo. Kwa njia hiyo ni lazima kujenga msingi
kwa vijana juu ya mazungumzo ambayo ndiyo nyenzo asili. Umuhimu wa mazungumzo umesisitizwa
pia Waziri wa Biashara ya nchi za nje Aphan Barry ambaye amesema kwamba, ndilo jambo
linakosekana kwa sasa , kwasababu hiyo inajionesha kutokana na vurugu na machafuko
mengi ya kikabila na dini. Anaongeza,”Furaha ya kuishi pamoja ndiyo urithi wa Burkina
faso. Utamaduni na dini zetu vina thamani ambavyo vinawawezesha kushinda mambo mengi
na kuleta maelewano”.
Pamoja na wengine waliyo toa hutuba katika Jukwa hilo , ni pamoja na mwakilishi wa
UNESCO na Fiermini Eduardo Matoko Mkurugenzi Mkuu akikumbusha , lengo la miaka 10
ya Kimataifa kwa ajili ya kukaribia utamaduni ;ni azimio lililotolewa na Umoja wa
Mataifa kuanzia mwaka 2013-2033,lilo jikita juu ya utofauti wa utamaduni, kabila,
lugha na dini kwa kuhamasisha mazungumzo.Katika jukwaa hilo, pia kazi za makundi na
kushirikishana wawakilishi wa taasisi, madhehebu mbalimbali walishiriki kikamilifu.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |