2017-03-10 16:30:00

Mafundisho ya Padre Michelini hakika ni mlima wa kutafakari!


Baba Mtakatifu Francisko baada ya kumaliza mafungo ya Kiroho Ijumaa asubuhi ya tarehe 10 Machi 2017 ametoa hotuba kidogo ya kutoa shukrani kwa Padre Julio Michelini aliye waongoza kwa tafakari ya mafungo yao na kusema , anapenda kumshukuru kwa mema aliyo watendea na zaidi namna alivyo jionesha kwao , kama asili kwa maana ya ukawaida japokuwa  yeyey ana uzoefu wa taalumua  yake ya  kimasomo , uandishi wa vitabu, marafiki wazazi, vijana , ndugu zake wadogo wa jumuiya anao ishi nao .
Pili Baba Mtakatifu Francisko anamshukuru kwa kazi aliyo ifanya na jinsi alivyojiandaa.Hii ina maana ya wajibu, yaani kuchulia mambo kwa uzito unaostahili.Anamshukuru kwa yote aliyo wajalia na kusema, hakika ni kweli kuna mlima wa mambo ya kutafakari , lakini  pia anakumbusha kuwa Mtakatifu Ignatius anasema wakati wa mafungo ukijisikia faraja au ukiwa ni lazima mambo hayo kuacha hapo,usisonge nayo mbele .Kwa hakika kila mtu ameweza kupata moja au mawili kati ya hayo yote.

Licha ya hayo siyo kupoteza , inabaki, itatumika kwa wakati mwingine: na pengine ni mambo mihimu na yenye nguvu, kwa wakati wengine haiwagusi chochote . labda ni neno dogo tu linaloweza kujikita zaidi.Anatoa mfano baba Mtakatifu Francisko, kama muhubiri mmoja wa Kihispania baada ya kutoa mahubiri yake  makubwa na aliyo kuwa ameandaa vizuri ,Mtu mmoja alimwendea na mdhambi akiwa na machozi akamwomba aweza kuuungamishwa . Alimuungamisha dhambi nyingi na machozi mengi. Muungamishi huyo alibaki kinywa wazi kwasababu alikuwa anafahamu maisha ya mtu huyo.Wakati huo alimuulizia niambie ni wakati gani umesikia kwamba Mungu amekugusa moyo wako?, na ni katika neno gani?. Aliposikia maneno hayo, yeye alianza kucheka , na wakacheka wote, kwa namna hiyo wakati mwingine maneno rahisi ni yale yanayotusaidia au yale magumu zaidi, kulingana na Bwana anavyotoa neno mwafaka .
Shukrani nyingi na uendele kufanya kazi kwa ajili ya Kanisa ,ndani ya Kanisa na kutoa mafundisho ya neno kwa mambo mengi ambayo Kanisa linakukabidhi. Lakini zaidi matashi mema ya kuwa ndugu mwema.

Sr Angela Rwezala

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican








All the contents on this site are copyrighted ©.