2017-03-06 16:08:00

Mafungo ya kiroho ya Baba Mtakatifu kuongozwa na Injili ya mateso


Jumapili 5 Februari 2017 kwenye nyumba ya mafungo ya kiroho iliyoko mji wa Ariccia Roma , Baba Mtakatifu Francisko amaeanza mafungo akiwa pamoja na  Sekretarieti Kuu ya vatican .Katika mafungo hayo kutakuwa na mada tisa za tafakari ya kwaresima , inayo ongozwa na Padre Giulio Michelini wa Shirika la ndugu wadogo wa Mtakatifu Francisko ambapo anawaongoza  katika kutafakari mateso , kifo na ufufuko wa Yesu Kristo kutoka katika Injili ya Mathayo . Baada ya utangulizi wa mafungo Jumapili jioni, sikiu yaJumatatu wameanza na tafakari ya Petro kumkiri Yesu wakati wako njiani kuelekea Mji wa Yerusalem.Hata hivyo Baba Mtakatifu Francisko aliomba asindikizwe kwa sala na kwa ajili ya wenzake , kwa kipindi chote cha mafungo ambayo yatamalizika tarehe 10 Februari  2017 wakati wa kumaliza sala ya malaika wa Bwana na salam zake Jumapili 5 Febuari 2017.Taarifa inasema kuwa kwa kipindi chote cha mafungo, mikutano mbalimbali na hata katekesi ya jumatano ya Baba Mtakatifu vitakuwa vimesitishwa.

Kwa mtazamo wa mateso kama ilivyondikwa na Mtakatifu Mathayo , itakuwa na kama vile kukaa mbele ya picha kubwa , kuitazama kwa pamoja ambapo labda inaweza kujikita ndani ya moyo kwa kitu fulani.Hayo ni maelezo ya Padre Padre Michelini kwa utangulizi wa mafungo  anaelezea juu ya kitabu fulani toleo mwaka 2010 kinachoelezea juu ya vifo vya kijujuu kwa watu wa kihistoria.Lakini anasema katika Injili zote zinaelezea kwamba Yesu alikufa kweli na maisha yake siyo film .Maisha na kifo cha Yesu kwa hakika ni vitu viwili sambamba. Kwa namna hiyo kila tafakari  kwa siku hizo  itaanza na sehemu ya Injili ya Matayo juu ya mateso , kifo na ufufuko , kwa mtazamo wa kina wa maisha yake ya kitume aliyo fanya huko Galilaya.
Aidha anasema , katika mafungo ya kiroho katika siku hizi pia ni namna ya kukaa na Mtakatifu Petro.Kwa njia hiyo inabidi kufuata maelekezo ya “Injili ya furaha” , mahali ambapo Baba Mtakatifu Francisko anawaalika wakristo  kukutana na Yesu mwenyewe  .

Kwa siki hizi Padre Michellini anatoa ushauri kwamba hata sisi sote  tunaweza kufikiria kwamba wote tuko ndani ya kikundi cha wale wanao paswa kuinjilishwa .Siyo kwamba tuko katika tabaka la wasio mtambua Yesu ,na wala  waliomo ndani ya wale walio batizwa ambao lakini wanaishi na mahitaji ya ubatizo, bali ni wale ambao uinjilishaji mpya umefikiriwa hawali ya yote kuwasha moto katika mioyo ya waamini ambao daima wako ndani ya jumuiya na wanafuata jumuiya .Padre Michellini anasisitiza zaidi akisema ni nyinyi ndugu mlio kiini cha unjilishaji , kwa papa , Sektratarieti ya Vatican katika kiindi hiki mwafaka ,na wote mnaalikwa kukaa pembeni na kusali.

Tafakari ya Padre Michelini ilianza na kwa kumtazama Mtakatifu Francisko wa Assisi alipo toa mahubiri  kwa Papa Onorio wa II na makardinali Mwandishi Tommaso wa Celano anasimulia ya kwamba askofu wa Ostia alikuwa na hofu ya kwamba Mtakafifu Francisko wa Asisi angeweza kudharauliwa kwa maneno yake rahisi wakati wa kutoa mahibiri kwa Papa na Makardinali na kwa njia hiyo Padrea anasema naye kidogo ana hofu lakini ataweza kufanya awezacho , maana mahali amabapo hawezi fika Roho Mtakatifu atafanya hivyo.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.