2017-03-02 14:49:00

Vyama Katoliki kupinga Kampeni za utoaji mimba Afrika


“Nchi za Magharibi hawakuwahi kuwa na mawazo ya kuuliza Waafrika wanataka nini.Huo ni ukoloni mamboleo.Ni utamaduni wa ubeberu , ni udikteta wa wafadhili matajiri” Huo ni ujumbe unaonekana katika Video ya Obianuju Ekeocha Rais wa Utamaduni wa maisha ya Afrika, ambao umeonekana hivi karibuni kwa kupinga maandalizi ya mkutano wa tarehe 2 Mach 2017 huko Brussels unao husu ufadhili wa kutoa mimba.
Mkutano huo wenye kauli “Yeye anachagua”umeandaliwa na nchi nne za Ulaya ikiwa ni Belgium, Denmark, Uholanzi na Sweden.Ni mkutano wenye lengo la kukusanya fedha kwa ajili ya  utoaji mimba katika nchi zinazoendelea ,mara baada ya Marekani pamoja na kuanzishwa sera mpya ya mji wa Mexico, ambao wanatoa kiasi kikubwa cha ufadhili kwa mashirika yanayotoa huduma za utoaji mimba nje ya nchi.


Hata umoja wa Ulaya utakuwa na wawakilishi  katika mkutano huo.Shirika la habari la SIR  limemnukuu Maria Hildingsson, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Kifamilia Katoliki (Fafce),vinavyo jihusisha juu ya mahusiano ya afya ya uzazi ambapo pia uingia hata kipengele cha utoaji mimba ,akisema “hiyo siyo sehemu ya Umoja wa nchi za Ulaya kutoa utatuzi kama ilivyokuwa imetolewa mwezi Desemba 2013.
“Kuna sauti nyingi za waafrika na Ulaya wana omba msaada wa kuboresha usalama wakati wa kujifungua na kusaidia afya ya uzazi , lakini si kwa ajili ya utoaji mimba”, anasema Hildigsson,nakuongeza akikimbusha juu milioni mbili za saini zilizoanzishwa kwa ajili ya maombi yao katika Tume ili  wasitishe kutoa fedha za msaada unaojihusisha na utoaji wa mimba.
 

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.