2017-02-23 16:41:00

Ni muhimu kujikita katika uchumi umoja ili kujenga maisha jamii


Ili wahamiaji wapate kubadilika na kuhitahiji fursa , amani na maendeleo ya pamoja katika familia ya binadamu.Ni matashi mema ya Katibu Mkuu wa Vatican Petro Parolin wakati wa hotuba yake Jumatano 22 Februari 2017 kwenye Jukwaa la VI la Kimataifa juu ya Wahamiaja na Amani kwa kaulimbiu “ushirikishwaji na maendeleo: kuanzia mwanzo hadi kufikia matendo”.Jukwaa hili limeandaliwa na Baraza la kipapa la Vatican la  maendeleoo na binadamu,Mtandao wa Kimataifa wa Shirika la Scaribian kwa wahamiaji na Chama cha Konrad Adenauer.


Kardinali Pietro Parolin anakumbusha juu ya Baba Mtakatifu Francisko anavyotia moyo kila anapopata fursa na kuwataka wote  kuchukulia hatua ya matukio haya ya wahamiaji , ambayo ni mojawapo ya matatizo ya msingi katika ulimwengu wa sasa.Katika ulimwengu wa sasa , ambao unatawaliwa na utandawazi ,unahitaji nguvu ya pamoja katika  kuonesha jinsi gani amani , maendeleo na kuheshimu haki msingi za binadamu inawezakana kwasababu kwa sasa imeanza kuonekana ishara msingi katika juhudi kwa maana ya mahusiano kati ya nchi na kati ya watu.
Kardinali anayataja matatatizo mbalimbali na mengi kama changamoto ya sasa akisema ni pamoja na sera za kisiasa kupenda kujinufaisha kwa riba na pia ishara ya hofu ya siasa za kutatanisha mipango,vilevile maendeleo ya chini na mageuzi ya matumizi ya fedha,na lengo la kuondokana migogoro isiyo kuwa na mwisho, ukiukwaji wa haki za binadamu, wasiwasi wa madhala ya mabadiliko ya tabianchi, na migogoro ya kiuchumi hayajatatuliwa , suala la itikadi kali pia misaada ya kibinadamu,kuzorota kwa kisiasa,kijamii,kibinadamu,kimazingira, na biashara ya jinai ya watu.Haya ni baadhi ya mambo yanayosabisha uhamiaji na zaidi pia kuwa vikwanzo na belia kwa upande wa siasa ya wahamiaji,  kuongeza njia mbadala na zaidi ni hatari kwa wahamiaji wasio kuwa na vibali  kuingia mikononi mwa  unyonyaji na unyanyasaji kwa upande wa watu wahalifu, na kusabisha maisha ya binadamu kupotea.


Karidinali Pietro Parolin anaongeza pamoja na  uhalifu huu, bado  kuongezeka tena matatizo mengine ya wahamiaji ambayo yanakuwa mizigo katika nchi nyingine,mahali ambapo uchumi na siasa huko hatarini, na ambapo nchi hizo haziwezi kukabiliana au kuhakikisha haki msingi za watu, au kulinda heshima ya utu wao vinatekelezwa.Pamoja na hayo pia Kardinali anasema uhamiaji kimataifa , haiwezi kufikirika kwamba ni dharura ya mpito tu , bali ni haki ya binadamu ya kuwalinda,na ni chombo ambacho kinapaswa kutazama kwa ujumla katika bara na kukabiliana na sababu zake kwa kutafuta mikakati ikiwemo ushirikiano kwa upeo wa pamoja kiulimwengu kwani anasema "ipo haja ya ushirikiano katika ngazi zote, kutokana na uchunguzi wa matatizo ya sasa na mapungufu ya kila nchi kwa kukabiliana peke yake na changamoto hii kubwa kwa jumuiya ya kimataifa kwamba, katika nafasi ya kwanza, lazima lengo la kuhakikisha watu na amani ya mtu binafsi na maendeleo, katika kufanya uhamiaji unakuwa ni chagua badala ya kuwa lazima.


Kwa ujumla Kardinali Pietro Parolin anahitimisha hotuba yake akisema ni lazima kujikita katika uchumi umoja ambao unajenga maisha kwasababu unashirikisha  masikini, hutumia faida katika kujenga umoja,na unaweza kuleta matumaini katika ulimwengu ambapo pia ni njia ya  kukutana,na kuleta matumaini mapya,heshima,utajiri wa mahusiano ambapo hata fedha kwa mtazamo wa kubadilishana zawadi,unaingia kaitka mzunguko wa mara mia kama ilivyotajwa hata katika Injili na kwamba "kwa yule anaye toa na anayepokea"ili  furaha iweze kuwa kwa wote.  

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.