2017-02-20 16:37:00

Baba Mt. Francisko anasema kulipiza kisasi siyo tabia ya ukristo


Injili ya Jumapili kutoka (Mt 5,38-48) ni kurasa ambazo zinajieleza vema kuhusu mapinduzi ya kikristo,kwani Yesu anaonesha njia  ya haki ya kweli ya kwamba upendo uzidi sheria ya  mkato wa ncha kali, yaani jicho kwa jicho na jino kwa jino.Sheria ya zamani ilikuwa kama vile ya kulipiza kisasi, adhabu ya kifo aliye kuwa ameua au kukatwa miguu aliyekuwa amedhulu mwingine.Yesu hataki mitume wake wapokee mabaya, bali nia yake ni kwamba nao waingilie kati bila kufanya ubaya wowote kujibu vibaya, siyo kuvunja mnyororo wa ubaya, ni sawasawa na kuendeleza ubaya huo.


Ni tafakari ya Baba Mtakatifu Francisko aliyoitoa Jumapili 20 Februari 2017 kwenye uwanja wa Kanisa kuu Mtakatifu Petro mjini Vatican wakati wa sala ya Malaika wa Bwana.Baba Mtakakatifu anaonya kulipiza kisasi bali kujaribu kukwepa visasi hivyo ikiwa njia ya ukristo wa kweli. Anasema,iwapo  kuna uwezekano wa kuvunja mnyororo wa ubaya , ni hakika kweli mabadiliko kuwapo.“ Ubaya kwa hakika ni utupu na haiwezekani kujazwa na utupu, bali kwa ujazo, maana yake kwa wema".Tabia ya kulipiza kisasi siyo soluhisho la migogoro. Akitoa mfano, umenifanyia mabaya nawe utakiona! hiyo tabia haitatua matatizo, na siyo tabia ya kikristo.
Kitendo cha Yesu kukataa vurugu ni njia ya kusema kwamba inahitajika haki halali, akitoa mfano ya wa kugeuza shavu la pili, wa kutoa mavazi au kujitoa sadaka mwenyewe. (Mt 5 39-42.).Lakini  kujikatalia mambo hayo haina maana kwamba hakuna haja ya kufanya haki isitendeke la hasha! ,kinyume chake ni upendo wa Mkristo unajionesha kwa namna ya pekee ya huruma na kuwakilisha utambuzi mkubwa wa haki.

Yesu anataka kutufundisha njia sahihi ambayo tunatakiwa kufanya  ya kutofautisha  haki na kulipiza kisasi.Kulipiza kisasi Baba Mtakatifu anasema kamwe siyo haki.Wajibu wetu  ni kufanya uadilifu wa kutafuta kutenda haki na kukatazwa kulipiza kisasi kwa njia yoyote na hata kwa kuchochea kisasi kwa maana ni aina ya chuki na vurugu.
Yesu hataki kupendekeza utaratibu mpya wa serikali,badala yake ni  amri,ambayo pia ni pamoja na upendo kwa maadui wa mtu isemayo "wapendeni adui zenu na kuwaombea wale wanaowadhulumu ninyi" (i44). Na hii si rahisi!.


Lakini Neno hili lisieleweke kama mhuri wa uovu unaofanywa na adui,bali kama mwaliko na mtazamo wa upeo wa juu wa ukarimu sawa ule wa Baba Yetu aliye mbinguni, ambaye Yesu anasema “huchomoza jua juu ya watu wabaya na wema,na uwanyeshea mvua wati wanyofu na waovu"(45). Hata adui kiukweli ni binadamu aliyeumbwa kwa mfano wa Mungu hata kama sasa amefunikwa na kivuli cha maovu na kuonekana hastahili.
Tunaposema maadui, tusifikirie  juu ya nani ambaye ni tofauti  na kuwa mbali na sisi, tunajadili kuhusu sisi wenyewe, ya kwamba tunaweza kuingia kwenye mgogoro na majirani zetu,wakati mwingine pamoja na familia.Swali, ni maadui wangapi ndani ya familia, tufikirie hilo! Baba Mtakatifu Francisko anatoa mifano mingine ya kwamba,maadui pia ni wale wanaosema vibaya juu yetu, wanao wasingizia wengine, na kutufanya vibaya.Hiyo si rahisi kumeza anadhibitisha .Kwa wote wanaitwa kukabiliana nao kwa wema , kwa maana ni mojawapo ya mikakati inayo ongozwa na upendo.

 

Bikira Maria atusaidie kumfuata Yesu juu ya njia hii ngumu, ambayo dhati  huongeza heshima ya binadamu na kutufanya kuishi kama watoto wa Baba yetu aliye mbinguni.Atusaidie kufanya mazoezi ya uvumilivu , mazungumzo , msamaha, na hivyo kuwa mafundi stadi wa umoja na ndugu zetu katika maisha yetu na hasa kuanzia ndani ya familia.


Baada ya sala ya malaika wa Bwana, Baba Mtakatifu aliwahutibia mahaujaji wote katika viwanja vya Mtakatifu Petro akisema: 
Anasitikitishwa na habari zinazoendelea kutolewa za mapigano na vurugu na ukatili katika Mkoa wa Kasai ya kati nchi ya Jamuhuri ya kideomkrasia ya Congo.anasema Baba Mtakatifu kwamba anahisi maumivu makubwa kwa wathirika na hasa watoto wengi ambao wametolewa kwa wazazi wao na katika shule, ili kwenda kutumika kama asikari. Hili ni janga la watoto kuwa maaskari!

Anawakikishiwa ukaribu wake kwa maombi yake , hata kwa ajili ya wafanyakazi wa dini na mashirika yasiyo ya kiserikali ambao wanafanyaka kazi katika ukanda huo  mgumu .Anarudia kwa upya kutoa wito wa dhamira kwa viongozi wa Taifa  na kwa jumuiya za kimataifa , ili kuchukua maamuzi sahihi kwa wakati ili kusaidia ndugu wanaozidi kuteseka.


Halikadhalika Baba Mtakatifu anaomba kusali kwajili ya watu wote hata katika sehemu nyingine za Bara ka Afrika na ulimwenguni wanaoteseka kwa sababu ya vurugu na vita.Akitaja nchi ya Pakstan, Itaq ambao wanazidi kukumbwa na vitendo vya ukatili wa kigaidi siku zilizopita. 
Baadaye aliomba kubaki kimya kwa kitambo baadye sala ya salam Maria .
Alimazia akiwasalimia wote mahujaji kutoka sehemu mbalimbali za dunia na mwisho kuomba sala kwa ajili yake .








All the contents on this site are copyrighted ©.