2017-02-16 14:39:00

Tutafuta mbinu mpya ya kuongea na vijana kwa mantiki ya lugha pia


Maadhimisho ya Sinodi ya Maaskofu kwa ajili ya vijana kwa Mwezi Oktoba, 2018 yataongozwa na kauli mbiu “Vijana, Imani na mang’amuzi ya Miito”.Maandaliz hayo yameanza kwanza kutoa hati ya maandalizi ya Sinodi ya XV .Kwa maandalizi ya hati hiyo nikutaka kuangalia vijana wote duniani katika utambulisho na ushiriki wao katika maisha yao binafsi .Pamoja na taasisi katika mchakato wa kuunda vijana wa kizazi kipya.Tunaweza kusema ni ramani zaidi kama tusomavyo kwenye utangulizi wa hati hiyo ambayo inajikita kwa undani zaidi kwa vijana katika mang’amuzi ya.
Hali kadhalika hati hiyo inatazama kwa mapana shughuli za kichungaji kuhusu miito na kuwataka viongozi wa Kanisa kufanya hija na vijana kuwasindikiza na hatimaye waweze kugundua, kuona na kuitikia wito wa kumfuasa Kristo Yesu.Kwa njia hiyo ni dhahiri kuona walengwa ni vijana wote pasipo kubagua na familia kama kiini cha miito , watu ambao wawe mfano bora wa kuigwa.


Pia kuna katika hati hiyo bado inaonesha sekta ipi vijana wanapendelea hili Kanisa liweze kushughulikia kikamilifu katika kazi ya kichungaji kwaaili ya  miito.Sekta hiyo ni katika mitandao ya kijamii ambap Kanisa linapaswa kujitahidi kuwakuta ili kuwaongoza Vijana
Mwandishi wa habari za Radio vatican, alifanya mahojiana na Kardinali Lorenzo Baldisseri Katibu mkuu wa Sinodi ya Maaskofu kuhusiana na hati hiyo ya maandalizi na kuchambua kwamba , Sinodi hii ni kutaka kwa dhati  kuwahusisha vijana kutokana na kwamba mara nyingi kuna misemo inayo sikika , vijana ni wadhaifu,vijana ni wenye matatizo. Anasame ni lazima kutambua ya kwamba vijana ndiyo mpango wa maisha endelevu na kwa hiyo ni vijana wa maisha hata ya  ya sasa. Ni wajibu wetu  kutambua hilo, kuwapa fursa na vipaumbele zaidi kama wahusika wakuu katika maisha yao ndani ya kamii.
Watu wazima ,hatulazimiki kuwapinga  mawazo yao , bali mi muhimu kuwasindikiza , kuwatia moyo, kuwashauri,  kama kwa mfano “ tazama vijana maisha ni kuwajibika, ni kazi ,lakini ni uzuri ni furaha, aidha tazama vijan, tunataka ya kwamba mtambue vema furaha ambazo sisi tunawalekeza ni kutokana na uzoefu wetu,kwa utulivu pokeeni ili nanyi mpate kukubali na kuwajibika katika kujenga maisha yenu ya leo na endelevu.


Hali kadhalika anasema ya kwamb Sinodi itawasikiliza vijana kwa ajili a kuwawezesha uwezo wa kujieleza wao wenyewe na kubadilishana  mawazo yao kwa wengine yale yatakayo kuwa maisha yao endelevu.Katika Hati ya maandalizi kuna kipengele ambacho kinaleza juu ya njia zilizotumika zamani ya kwamba  hazifanyi kazi tena, kwasababu uzoefu wa kizazi kilichopita, kinaonekana kupitwa na  wakati kwa haraka. Kwa njia hiyo inabidi kutafuta mbinu mpya za kuwashirikisha vijana ,kitu ambacho kwa hakika Sinodi ya vijana ndiyo kazi inayotakiwa kufanya.
Kardinali Baldisseri anasema  kwa  hakika Sinodi inataka kutafuta  hawali ya yote lugha ya kutumia kwaajili ya kuwasindikiza vijana.Lugha ambayo inawezesha vijana kuelewa kwa haraka kutokana na mabadiliko ya  kukua kwa kwa haraka  kwani mara nyingi inakuwa vigumu kueleweka kwa watu wazima,na kwa njia hiyo husababisha hukuma siziso na msingi , hivyo mbinu zilizotumika za kizamani lazima kubadilishwa na kuweka mwendelezo wa mbimu mpya ambayo itawezesha kueleweka kwa wote na kuifuata.

 

Kardinali pia anaelezea juu ya Sinodi hii kuwa na mitazamo ya wosia wa kitume wa “Furaha ya Injili” na “Furaha ya Upendo”na kusema katika wosia hiyo wito wa neno la vijana limetamkwa mara 36 , na kwa njia hiyo ni kupata kielelezo cha kuweza kueongelea mada hiyo kwa vijana . Ni dhahiri ya kwamba familia ndiyo msingi ambapo umeongelewa kwa miaka hii mitatu.Na kwasasa  lakini mababa wa Sinodi wataongea mada ya vijana .Na hiyo ni hja kubwa ya kuengea mada hii kwasababu ya mwendelezo wa mada ya familia ambapo ndiyo umekuwa mpango wa Baba Mtakatifu Franciko.Kwa upande wa (Evangelii Gaudium) “Furaha ya Injili” tunakutana na mada zote , hati hizi mbili ni muhimu  kwa ajili ya kuelewa zaidi kile kinachotendeka kwa sasa:na kwa njia hiyo maandalizi ya hati ya vijana italeta matokea mengine baadaye wakati ikifika muda wakufungua Sinodi hiyo.

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican








All the contents on this site are copyrighted ©.