Baba Mtakatifu Francisko amemteua Askofu Mkuu wa Warsaw -Praga nchini Uholanzi Henryk Hoser, S.A.C. kuwa mwakilishi wake maalum huko Medjugorje nchi Bosnia. Nia ya Baba Mtakatifu kumtuma huko ni kuangalia mahitaji ya mahujaji wanao kwenda huko. Kutokana na wingi wa watu hao , anakwenda kuona shughuli za uendeshaji wa shughuli za kichugaji na ikibidi kutoa ushauri kwaajili ya maendeleo endelevu ya shughuli za Kanisa katika uchungaji.
Pamoja na ziara hiyo, Askofu Mkuu Henryk Hoser, S.A.C. ataendelea na shughuli zake za kichungaji katika Jimbo lake Kuu Warsaw - Praga wakati huo huo akiendelea pia na utume alio takiwa na Baba Mtakatifu hadi atakapomaliza utume huo wakati wa kiangazi mwaka huu.Ikimbukwe kwamba ni maelfu na maelfu ya watu wanaelekea katika eneo hilo kwaajili ya kusali katika Kanisa la Maria wa Medjugorje nchini Bosnia Ulaya ya Mashariki.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya radio Vatican.
All the contents on this site are copyrighted ©. |