2017-02-12 13:37:00

Miaka 88 ya mkataba wa Laterano kati ya Kanisa na nchi ya Italia


Ni miaka 88  ya mkataba wa Laterano kwasababu tarehe 11Februari 1929 Kanisa Katoliki na Serikali ya Italia ,walitia saini a mkataba wa makubaliano ya masuala ya ushirikiano katika utendaji wa shughuli za utume wa Kanisa. Vilevile mwaka huu unakwenda sambamba na uhusiano muhimu wa tukio la ishara ya mwisho kuhusu mji wa Roma, kwa njia hiyo ni tukio la upatanisho kati ya Kanisa na Serikali ya Italia ambapo ulikuwa ni uzinduzi wa kushirikiano kati yao.
Kwanza inabidi kukumbuka sheria ya Kanisa kupitishwa ,ambayo ni ya kwanza katika historia ya Kanisa kwa kupitia kazi ya mikono ya Papa Benedikto wa XV mwaka 1917.Ni sheria iliyo anzishwa  kwaajili ya kukidhi haja ya kiu katika ngazi ya kichungaji na Papa Pio wa X kwaajili ya kusaidia Kanisa waingie bahari ya kisasa na kuunga mkono shughuli za kichungaji kwenye  kupiga makasia katika bahari mpya na ngumu.


Kwa mtazamo wa hatua za historai hiyo ni kwamba Sheria hiyo ilijitokeza wakati wa  kipindi ambacho Serikali ilikuwa imewatoa  nje  Kanisa  wasiwe na haki ya sheria katika mfumo wa raia,ki ukweli hali hiyo ilileta matatizo makubwa ya maisha ya Jumuiya ya Kanisa , ambayo ilikuwa inaishi na inaitwa kuishi katika watu wa nchi hiyo ya Italia. Halikadhalika  Kanisa ilikuwa inajikita kutoa ishara kubwa na manufa ya wote kama vile ukombozi kutokana na madai ya kale na sheria za kiserikali.Kwa njia hiyo Kanisa liliweza kijipanga kisheria kutokana na uwezekano wa binadamu, kwa ajili yake , na kuwa na haki katika katiba na uhusiano na mwisho kwa kila mtu.

 
Kwa muonekano zaidi tunaweza kusema kwamba sheria ilionesha ni muhimu kwa Kanisa walioitwa kukukabiliana  na upungufu wa demokrasia , na upinzani katika ujio wa udikteta kwa wakati huo .Na katika hatua hii ni dhahiri kwamba makubaliano ya mkataba wa Lateran ,ilitokea wakati wa matukio ya  nchi   na kufungua mlango wa Porta Pia tarehe 20 Septemba 1870, kwa njia hiyo ilikuwa na matunda ya mkataba huo kwasababu nyuma kulikuwa tayari kuna nyenzo za kisheria zimepagwa vizuri.
Maadhimisho ya pili ni yanahusiana na kuzaliwa kwa Jamhuri ya nchi ya Italia , baada ya mwisho wa udikteta na vita.Kipndi hicho kilitawali na maadili ya juu na mawazo motomoto licha ya kwamba kulikuwa na  utofauti katika nafasi za kisiasa ambazo zilikuwa zinafanya umoja wa Italia kuwa mgumu katika kutafuta ukombozi.

Kukumbuku hiyo ya Katiba ambayo  ilipitishwa tarehe 22 Desemba 1947 ikaungwa mkono na idadi kubwa ya watu na kuanza mara moja kwa kasi zake tarehe 1 Januari 1948.Katiba hiyo kwa hakika  inatoa kipengele  katika haya ya pili Ibara ya 7 ambapo mkataba wa Lateran , kwa dhati unathibitisha.Kwa mtazamo huo ni kushukuru kufanyika marekebisho yalikuwa yamekubaliwa katika mkataba kwenye  makao makuu ya serikali ya Italia Villa Madama ya mwaka 1984. Mikataba hiyo imeweza kuendelea kukuana nguvu chanya zilizopo katika vifungu vinavyo husika.
Lakini wito mkuu wa Katiba kwa mtazamo wa mahusiano yaliyopo kati ya Kanisa na Serikali unaleta maana zaidi, kwasababu vipengele kadhaa kama vile nafasi ya maadili, juu ya utaratibu wa sheria ya Italia na maadili ya kijamii ambayo ni kanuni ya pamoja na wote,vilevile  kuanzisha umuhimu wa binadamu na hali zake  , utu wa binadamu , na kanuni ya misingi ya mshikamano.

 

Halikadhalika katika uwanja wa matukio ya dini, uwepo wa uhuru shirikishi, kitaasisi na uhuru wa raia bila ubaguzi , wakati huo kwaajili ya kushirikiana kati ya Kanisa na Serikali ili kukuza wema wa binadamu kama isemavyo Katiba Ibara ya 1 ya mkataba huo. 
Aidha unahusu ushirikiano ambao ni alama ya miaka mingi bila kuwa na utata wa majukumu na shughuli, katika kuhamasisha  ukuaji wa nchi katika masuala ya zana na maadili,ambao kwa mara nyingine tena ,umepata nafasi za kujieleza katika nchi kwa mantiki ya asili ya mkataba ambao unaadhimishwa miaka 88 japokuwa katika uchungu wa matukio mbalimbali yaliyo jiokeza hivi karibuni , na ambayo kwa kiasi kikubwa ni wa  kusikitisha na  kugusa watu wengi Italia na pia kusikitishwa na maisha ya jumuiya nyingi kwa ujumla.

 

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican








All the contents on this site are copyrighted ©.