2017-02-10 16:49:00

Usitoe nafasi ya mazungumzo na shetani, utaanguka dhambini


Kwa neema ya Yesu , itusaide tusifiche udhaifu na vishawishi vyetu tilivyo navyo  bali tuombe msaada wa kutuinua ili tuendelee mbele.Ni maneno ya Baba Mtakatifu Francisko katika mahubiri ya Ijamaa 10 Februari wakati wa  Ibada ya Misa kwenye Kikanisa cha Mtakatifu Marta Mjini Vatican.
Akitafakari mwendelezo wa somo la kwanza kutoka katika kitabu cha mwanzo , sehemu ya  ya shetani akiongea na  mwanamke, ili aweze kuanguka katika dhambi kwa udanganyifu.Baba Mtakatifu anasema, vishawishi hupelekea  kujificha kwa Bwana na hivyo inakufanya kubaki mwenya dhambi, na udanganyifu .


Katika vishawishi na dhambi Baba Mtakatifu anatazama somo kuhusu Adamu na Eva na pia Maongezi ya Yesu  na shetani  jangwani, na kusema ni shetani anayeonekana kwa  mfano wa nyoka ,anatumia  ushawishi kwa maneno ya ulaghai , kwa maana yeye ni mtaalam, na ni baba wa wa uongo. Yeye anajua namna ya kulaghai, na jinsi gani ya kurubuni watu. Yeye alifanya hivyo kwa Eva kwa uongo wake, akaanza mazungumzo naye , hatua kwa hatua akampeleka mahali anapotaka yeye.
Kwa upande wa Yesu ni tofauti , anaeleza Baba Mtakatifu kwa sababu shetami alifika mahali pabaya.Alitafuta namna ya kuzungumza na Yesu , kwasababu shetani daima anapata kudanganya mtu kwa njia ya mazugumzo :anatafuta namna ya kundanganya , bali Yesu hakuweza kuanguka katika udanganyofu huo. Kwa naana hiyo shetani anajieleza mwenyewe, lakini Yesu pia anampatia jibu ambalo ni neno la Mungu. Kwa maana hiyo haitakiwi kabisa kufanya mazungumzo na shetani, la sivyo unataishia kuwa kama Adamu na Eva walivyo fumbuka macho na kuona utupu.


Shetani halipi vizuri, ni mdanganyifu, anatoa ahadi kwa yote na kukuacha utupu. Hata hivyo Yesu mwenyewe alibaki utupu msalabani , si kwaajili ya shetano bali kwaajili ya kumtii  Baba yake, lakini  hiyo ni njia nyingine.Nyoka ambaye ni shetani ni mjanja, huwezi kamwe kufanya mazungumzo naye. Wote tunatambua wazi vishawishi ni kitu gani , kwasababu wote tunashawishika, kwa mfano kuna vishawishi vingi kama vile kujipendekeza ,ubatili, kiburi, ulafi, uchoyo na vingine vingi Baba Mtakatifu anasema.
Leo hii watu wengi wanaongea suala la rushwa , hata kwa hilo tunapaswa kuomba msaada kwa Mungu,kwasababu kuna rushwa nyingi Baba Mtakatifu anabaninisha na kusema,kuna samaki wakubwa ambao wako duniani, ambao tunawasikia katika magazeti.Anatoa mfano ya kwamba ,labda walianza nao kidogo kidogo , sijuhi labda wakati wa kupima kwenye mzani, badala ya kufanya kilo moja wanaanza gram 900, ambayo inafanana na kilo moja.Rushwa huanza kidogokidogo kama vile mazungumzo ya shetani , akisema “siyo kwamba tunda litakuharibu , kula ni tamu!;kwa taratibu wakaanguka katika dhambi.


Kanisa linatufundusha tusiwe wepesi , usije ukasema ujinga, na hivyo Baba Mtakatifu anasema li lazima kuwa macho na kuomba kwa Bwana kwasababu peke yetu hatuwezi.Adamu na Eva walijificha kwa Bwana , lakini kinyume na sisi, tunahitaji neema ya Yesu ili kurudi na kuomba msamaha.Baba Mtakatifu anarudia kusisitiza tena ya kwamba katika vishawishi ni taadhali sana kufanya mazungumzo na shetani ,badala yake ni kuomba ukisema nisaidie Bwana , mimi nimdhaifu.Sitaki kujificha , na hiyo ndiyo ujasiri wa kushinda.Kwani ukianza  mazungumzo utaishia kushindwa . Kwa njia hiyo Bwana aweze kutupa neema ya katika safari kwa ujasiri ili tusipate kudanganywa katika udhaifu wetu na katika vishawishi. Atupatie ujasiri wa kuamka na kuendelea na safari mbele, na ndiyo maana Yesu alikuja kwaajili hiyo.


Sr Angela Rwezaula 
Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.