2017-02-08 16:39:00

Mahusiano ya Vatican na Japan ni historia ya utamaduni wa kale


Tangu tarehe 28 Januari  hadi yarehe 3 Februari 2017, Askofu Mkuu  Paul R. Gallagher , Katibu wa Mahusiano ya nchi za Nje wa Vatican , alifanya ziara maalum  huko Japan kwa mwalimko wa viongozi . 
Askofu mkuu akiwasili huko 28 akiwa amesindikizwa na Monsinyo Roberto Lucchini , mshauri wa Balozi katika ofisi ya Katibu wa nchi na kupokelewa uwanja wa ndege wa Narita na Askofu mkuu Joseph Chennot , Balozi wa papa wa kitume huko Japan na Balozi wa Vatican Askofu  Yoshio Matthew Nakamura , na Katibu wa Balozi wa Papa huko Japan  Mons. Paweł Obiedziński na wawakilishi wa Baraza la maaskofu wa Japan.


Siku aliyofika alipata kukutana na wawakilishi wa Kidplomasia wa serikali ya nchi akiwemo Waziri wa Uchumi  ,Nobuteru Ishihara,ambapo Katibu wa mahusiano na nchi za nje Askofu Mkuu Gallagher alielezea juu ya mshikamano na ushirikiano ambao ulianzishwa na mahusiano ya kale ya utamaduni na kiroho , na kwamba leo hii umepata kujieleza thabiti katika ahadi ya kueneza amani na pia kwaajili ya upungufu wa silaha za kinyukilia , na kwa kushirikiana na nchi zinazoendelea na kulinda mazingira.
Tarehe 29 Januari baada ya misa katika kanisa Kuu la Tokyo Askofu Mkuu Gallagher alikwenda Hiroshima , na tarehe 30 Januari katika omelia yake katika misa ya haki na mani iliyoadhimishwa katka Kanisa kuu la kumbukumbu , alipenda kumbuka historia ya ziara ya matembezi ya Mtakatifu Yohane Paul wa Pili aliyetamka kwamba amekwenda kama muhujaji.


Baada ya misa ya tarehe 31 Januri katika Shirika la wasalesiani Akabane kando ya mji wa Tokyo, Askofu Mkuu alikutana na Waziri mkuu  Shinzo Abe.Wakati wa mazungumzo yao walionesha ushirikiano mzuri kwa ngazi ya nchi zote mbili na haja ya  kutahidi kuwa pamoja katika maendeleo dhabiti na ya amani katika nchi. Hali kadhalika Waziri Mkuu alikumbuka kwa shukrani kupokelewa na Baba Mtakatifu  Francisko mnamo mwaka 2014 , ambapo alitaka kwa namna ya pekee amfikishie mwaliko wa maombi  ya ziara yake kwa niaba ya watu wa Japan.

 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.