2017-02-02 15:04:00

Ukeketaji bado ni tishio hata katika jamii ya wahamiaji Italia


Katika Jumuiya za wahamiaji wanaoishi nchini italia wapo wanawake wengi waathirika wa uketaji na asilimia kubwa inatofautiana kulingana na asili ya nchi yao. Makadirio ya mwaka 2016 inaonesha idadi ya wanawake wageni ,wamekeketwa ambapo ni wanawake kati ya 46,000 na 47,000  hizo ni takwimu zilizotokana na wanaweke vijana walio jifungua watoto  nchini Italia. Na zaidi ya asilimia 60 ya wanawake walio nchini Italia wameonesha kutoka  nchi ya Nigeria na Misri.
Lakini Ukifikiria  kiwango cha waathirika kwa ujumla ni wanawake kutoka nchini Somalia walio athirika zaidi ya  kwasababu ni asilimia 83,5% wakifuatiwa wanaotoka  Nigeria asilimia 79,4% na Burkina Faso asilimia 71%.Halikadhalika  jamii ya Misri (60.6%), Eritrea (52.1%), Senegal (31%) na Ivory Coast (11%).


Hayo ni baadhi matokeo ya utafiti uliofanywa na mradi wa Daphne MGF –PREV  unaoendeshwa  nchini Italia katika Chuo Kikuu cha Bicocca Milano kwa lengo la kikadiri ukubwa wa hali halisi ya watu walio pata uzoefu wa kuathirika na ukeketaji huo miongoni mwa jamii inayoishi katika nchi ya Italia.Matokeo hayo yaliwasilishwa tarehe 1 Februari 2017 kwenye Chuo Kikuu  Bicocca Milano katika Mkutano ulio andaliwa na Shirika la ActionAid na chama cha Utamaduni katika mtazamo wa Siku ya Kimataifa  ya kupinga ukeketaji wa wanawake, itakayo fikia kilele chake tarehe 6 Februari 2017.

 








All the contents on this site are copyrighted ©.