2017-01-31 14:22:00

Umoja wa Afrika kuanza juhudi ya mashirika ya ustawi endelevu



Mkutano wa 28 wa Umoja wa Afrika umeanza Jumatatu 30 Januari 2017 ambapo wanahudhuria wakuu wa nchi na viongozi wa serikali wa nchi 54 kutoka bara la Afrika. Viongozi hawa wanatazamiwa kujadili maswala muhimu yanayoigawanya jumuiya ya Kiafrika wenye Kaulimbiu "kupata faida kamili ya mgao wa watu kwa kuwekeza katika vijana. 
Maandalizi ya Mkutano huo yalianza 22 Januari 2017 katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa  na kikao cha kawaida cha Kamati ya wawakilishi wa kudumu (kuanzia tarehe 22 -24 Januari), ilifuatiwa kikao cha Baraza Kuu wakiwepo Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi wanachama (kuanzi Januari 25 hadi 27), na mwisho Kikao cha Wakuu wa nchi na viongozi wa serikali ambacho kimefunguliwa rasmi Jumatatu, Januari 30.


Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Ethiopia, serikali imetoa wito kwa jeshi ili kuhakikisha usalama umeimarika katika mji wa Addis Ababa wakati wa mkutano huo.Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Ethiopia amesema zaidi ya viongozi 4,000 wa ngazi ya juu wanatarajiwa kushiriki katika mkutano huo, ikiwa ni pamoja na Wakuu wa nchi na viongozi wa serikali 37 na Mawaziri wa Mambo ya Nje wasiopungua 49. 
Aidha katika ufunguzi wa Mkutano huo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika hotuba yake amesema kuwa umoja huo upo tayari kufanya juhudi za kuona amani inapatikana barani Afrika.Hali kadhalika Bwana Guterres ameashiria namna baadhi ya nchi za Kiafrika zilivyoshindwa kupiga hatua kubwa kiuchumi na kuongeza kuwa, umoja huo unafanya juhudi za kuanzisha mashirika kwa ajili ya ustawi endelevu katika nchi za Kiafrika.Vilevile Katibu Mkuu ameongeza kwamba, hitilafu zilizopo kati ya nchi za Kiafrika zinaweza kupatia ufumbuzi kwa njia ya mazungumzo kwa kuungwa mkono na nchi wanachama wa umoja huo na ule wa kimataifa.


Hali kadhalika Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António  Guterres amemhakikishia Rais John Magufuli wa Tanzania ushirikiano kutoka chombo hicho ikiwemo usaidizi kwenye tatizo la wakimbizi.Ametoa hakikisho hilo wakati wa mazungumzo kati yao, kando ya mkutano wa wakuu wa Muungano wa Afrika,AU huko Addis Ababa, Ethiopia.Amesema Umoja wa Mataifa utatia msisitizo zaidi katika kuhimiza wadau mbali mbali wa maendeleo wa jumuiya ya kimataifa kuchangia juhudi zinazofanywa na Tanzania za kuwapatia hifadhi wakimbizi wa nchi mbalimbali tangu mwaka 1971.
Kwa upande wake Rais Magufuli ameelezea juhudi za Tanzania na Jumuiya ya Afrika Mashariki za kushughulikia mzozo wa Burundi, akisema harakati hizo zinazoongozwa na Rais mstaafu wa Tanzania Benjamin Mkapa zinaendelea vizuri.

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.