2017-01-21 14:55:00

Maaskofu wa Rwanda kuandaa wiki ya familia na changamoto zake


Familia na changamoto zake ndiyo imekuwa kiini cha mkutano wa Kamati ya Baraza la maaskofu wa Rwanda kwaajili ya familia na Kanisa nchini humo.Habari kutoka katika mtandao wa Baraza la maaskofu wa Rwanda (Cepr) zinasema Kamati hiyo imekutana hivi karibuni mjini Kigali , na kungozwa na Askofu Antoine Kambana, Askofu wa Jimbo la Kibungo na rais wa Kamati hiyo.


Wakati wa kazi ya  kikao chao, waliteua kamati ndogo sita , na kila kamati iweze kuwajibika kwaajili ya kuchambua kila changamoto juu ya maadili ya ngono na familia, afya,vijana,wanafamilia kusindikizwa,sheria,na maadili mpya ya dunia.Mihimili mpya hiyo kwa sasa inapaswa kufanya kazi juu mpango wa mikakati mitano,kwaajili ya tume ili kukabiliana na mambo mengi kama vile itakadi ambayo inaweza kuharibu familia.Wanatoa mfano kwamba kuna baadhi ya mipango ya mafundisho  inayotolewa kwa mtazamo rahisi utafikiri ni muhimu na yenye manufaa , na kumbe ni kinyume kwani kuna vipengele vinavyopingana na maadili ya familia.


Pamoja na hayo Mkutano huo ulikuwa pia na hoja ya  maandalizi ya wiki ya familia ambayo inatarajiwa kufanyika kuanzia 13-19 Februari 2017. Nia ya maandalizi hayo ni kutaka kuhamasisha hisia na kutoa umuhimu wa familia, mahitaji yake ya haraka,kwenye usimamizi, thamani yake ya ndoa ya familia.
Aidha wameafikiana kufanya wiki hiyo wakati wa tukio la  sikukuu ya Mtakatifu Valentine ifanyikayo kila mwaka 14 Februari ili kuwawezsha kuhamasisha zaidi wakristo katika kuonesha upendo wa kweli na dhati wenye maana, ambapo kila parokia watatakiwa kuandaa  mpango maalumu na  wakati huo Baraza la maaskofu watatoa ujumbe wa siku hiyo.

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.