2017-01-19 16:20:00

Wanafunzi wa Italia kupendelea somo la mafundisho ya dini katoliki


Mafundisho ya dini katoliki  katika nchi ya Italia ni somo linalopendwa na vijana kwa asilimia 80% ya wanafunzi ambapo imeonesha kiwango cha asilimia kubwa hiyo  kutokana na takwimu za Taifa kuonesha  juu ya ufundishaji wa somo hilo la dini katoliki. Aliyatamka  hayo wakati wa kutoa toleo jipya la kufundishia Jumanne 17 Januari Roma na  Rais wa Baraza la Maaskofu Italia,Askofu Nunzio Galantino.


Mafundisho ya dini shuleni limechaguliwa sana  na wanafunz  kwani alisema kwani katika utafiti wa kitaifa inaonesha kwamba wapo walimu 3,000 wanao fundisha somo la Dini Katoliki na zaidi ya wanafunzi 20,000 wana udhuria katika somo hilo.Lakini pia askofu anasema kwa  miaka iliyopita ilionesha kushuka kwa kiasi japokuwa haikushuka sana.Pamoja na hayo inaonesha asilimia 91,7% ya wakufunzi wa somo hili wako katika shule za Serikali  na asilimia 56% wanafundisha  katika shule Katoliki, licha ya hayo  wanao udhuria somo la dini Katoliki ni wote hata  wale wasio wakatoliki.

Askofu Galantino  anasema; wakati mwingine somo hili la mafundisho ya dini katoliki, uonesha kupuuzwa na sehemu ya jamii, hiyo ni kwasababu  ya dunia hii tunamoishi ambapo kumekuwa na itkadi mbalimbali ambapo utoa ushawishi  wa kutupilia hewani kila kitu,ambacho hadi sasa kimetendeka. Pamoja na yote askofu anaeleza  kuna jambo  la kutia  moyo kwa ufundishaji wa  dini na hasa  kuona kwamba asilimia 67%ya  walimu wanaofundisha somo hili na wanatoa maana ya maisha  kwa vijana na zaidi ya asilimia 57% wanaunga mkono kwamba hii inasaidia katika kukabiliana na utamaduni.

 

Askofu Galantino pia anasema udhaifu wa somo hili la dini ni kutojua kutofautisha kati ya mafundisho ya dini na katekisimu , pamoja na kwamba asilimia 96% ya walimu ni walei .Alimazia akisema , mafundisho ya somo la dini katoliki au  mafundisho ya katekisimu siyo lengo katika shule za Umma za Italia,bali narudia kusema mafundisho ya dini katoliki ni mafundisho yanayo jikita kikamilifu katika mtaala wa shule , na kujikita   kikamilifu  katika hali ya utamaduni wa jamii ya Italia.

 

Sr Angela Rwezaula. 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.