2017-01-05 14:00:00

Wanawake wa Eritrea ni wafungwa Libia na waathirika mara mbili


 Habari kutoka kwenye Gazeti la Oservatori Romano , linatoa kisa cha wanawake wa Eritrea kufungwa huko Libya na kuwa waatihirika mara mbili. Kisa hicho kimetokana na vijana au watu wengi kiacha nchi zao wakifikiri wataweza kujikomboa kimaisha wakiingia katika nchi nyingine  lakini matokeo yake ni kama haya anayosimulia kijana wa kike  wa Eritrea.


Wered ni  msichana wa miaka 16 kutoka Eritrea alikuwa na  ndoto ya maisha yake ya baadaye ya kwenda Ulaya , akifikri angesoma, baada ya masomo angepata kazi, baadaye  angetengenza familia.Ndoto hizo pia zilikuwa  baada ya kazi ataanza  kuwatumia ndugu zake fedha za matumizi .
Baada ya  mwaka mmoja na nusu kupita aliamua kuondoka na kile alichokuwa amekwisha kusanya na kuwacha familia, mama  yake huko Eritrea. Alianza safari na kukatisha nchi ya Sudan hadi nchi ya Libia, fedha alizo kuwa nazo zilikuwa ni kuwapatia wafanya biashara haramu ya binadamu ili apate nafasi kwenye mtumbwi wa kuvumsha bahari ya Meditrenia(Bahari ya kati) na kufikia fukwe za  Lampedusa nchini Italia.


Mawazo yote hayo hayakufika mbali bali,kwani safari yake ilishia mpakani  wakati wa  ukaguzi kwenye kituo kimoja Ajdabja Libia ya mashariki, ambayo ni sehemu mojawapo yenye kupitiwa na  wakimbizi wengi wanapokuwa wakielekea forodha ya Tripoli.
Mpakani hapo kijana huyo alitekwa nyara  na kikundi cha wanaume akiwa pamoja na kikundi cha mwanawake zaidi ya 10 waliokuwa wakiongozana na safari yao ya kutafuta maisha, na kupelekwa  kwenye forodha za Sirte.Forodha  hizo zikumbukwe ni forodha alikozaliwa na kifo chake  aliyekuwa rais Ghedafi.Kwa mwaka mmoja sehemu hiyo ilitangazwa kuwa Serikali ya kiislam ya Isis, mji mkuu wa Tripoli.

Leo hii msichana Wered anao ujauzito , lakini hajuhi  ujauzito huo ni wa nani kutokana na kwamba, yeye na wenzake wameingizwa kwenye kwenye biashara ya ngono na wanajeshi wa Al Baghdad huko Libia. Akihojiwa na mwandishi wa habari, Wered anasema  "ameuzwa" anayasema hayo akiwa amefunikwa uso na kitambaa cha dhambarau, lakini kwenye macho yake inaonesha kweli  mateso yake na  mahangaiko.

Kijana anasema kutokana na kutokujua huyo mtoto ni wana nani na wala hajuhi ni miezi mingapi ya ujauzito , mtoto huo hamataki na kutamka  “ ni mtoto wa shetani” na kuendelea, "kwa miezi minne nimeuzwa kwa wanaume wa nne. Mpaka sasa ninaye mmoja wa nchi ya Sudan, ninachotamani tu ni kusahau , tamani kusahulika kabisa, kusahau  nilivyotumiwa kama jalala, kusahau nilivyo uzwa mara walipochoka kunitumia"


Aidha kijana wered alitoa ushuhuda wa vitendo vya vingi na vya  kutisha vinavyoendelea kuwapata na mateso makuu akiwa na wenzake kutoka Eritrea.Jinsi gani walivyoshurutishwa kuukana ukristo , wakielezwa na watesi wao ya kwamba wamepata kuwakata shingo wakristo wengi kutoka katika nchi yao, na kama hakubali kubadili dini yao nao wataishia kukatwa shingo mbele ya watu na kuwachoma.

Walikuwa wakikimbia umasikini, lakini leo hii wako kifungoni , wanakuwa waathirika mara mbili, hawawezi kufikia lengo lao, ndoto yao ya kufika Ulaya, licha ya hayo hawezi pia kurudi makwao kwasababu  wanasema upo uwezekano wa kuwawa.

 

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.