2016-12-30 16:00:00

Mwaka 2016 watu karibia milioni 4 wamehudhuria matukio ya Papa mjini Vatican


Katika tukio la kufunga mwaka , Msimamzi mkuu wa Nyumba ya kipapa , ametoa takwimu ya mahujaji walioweza kufika kwenye matukio mbalimbali yaliyoendeshwa Baba Mtakatifu Francisko mjini Vatican kwa kipindi chote cha mwaka 2016 ambapo watu 3.952.140 wameudhuria matukio hayo : Matukio haya  yanaunganisha matukio  makuu, maalumu, matukio ya Jubileo ya mwaka wa huruma , maadhimisho ya liturjia Takatifu, sala za malaika wa Bwana na katika sala ya  Malkia wa Mbingu. Lakini ikumbukwe kwamba , taarifa hizi za karibunini ambazo zimehesabiwa kutokana na tiketi zilizotolewa  na wasimazi wa nyumba ya kipapa, ambapo zinajumuisha, namba ya waamini walioweza kudhulia  vipindi vya sala ya malaika wa Bwana  au Sala ya malkia wa mbingu  zilizofanyika katika viwanja vya Mtakatifu Petro.


Zaidi ya hayo, takwimu  zinaonesha  miezi ambayo watu walikuwa wengi kama vile mwezi wa tatu, kutokana na uwepo wa  Juma Takatifu na pia Mwezi wa Septemba kwenye tukio la kumtangaza  Mama Theresa wa Calcutta kuwa Mtakatifu, na kufanya idadi ya watu 3.952.140. Takwimu hiyo inaonesha mikutano na  iliyofanyoka Vatican tu , kwa namna hiyo haionyeshi idadi wa maudhulio ya matukio mengine ya Papa aliyoweza kufanya ziara yake ya kichungaji  katika majimbo ya Roma na Italia kwa ujumla.Pia haionyeshi hata ziara za Kimataifa za kitume kama inavyosemekana kwamba Baba Mtakatifu alikutana na mamilioni ya watu kwenye maadhimisho ya  misa Kakatifu , ikiwa ni pamoja na watu wengi waliokuwa njiani wakimsubiri apite kwa mfano  (Mexico. Lesvos Ugiriki , Armenia, Poland, Georgia, Azebaigian ma Sweden.)

Sr Angela Rwezaula 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio vatican.








All the contents on this site are copyrighted ©.