2016-12-28 15:23:00

Papa Francisko: Imani ni mapambano katika majaribu!


Baba Mtakatifu Francisko katika katekesi yake ya kila Jumatano, na  iliyofanyikia katika ukumbi wa Paulo wa sita tarehe 28 Desemba 2016 ,  ametoa tafakari  juu ya imani na matumaini ya Abrahamu baba wa imani kutoka (Mw 15, 3-6). Alianza  kusema , katika Barua ya Mt. Paulo kwa warumi , inatukumbusha sura ya Ibrahimu baba wa imani , kwa kutuelekeza njia ya Imani na matumaini. Mtume Paulo  anaandika , “Abrahamu aliamini na kutumaini na hivyo amekuwa baba wa mataifa mengi kama maandiko matakatifu yasemavyo “wazao wako watakuwa wengi kama nyota” (Rm 4,18). Mtakatifu Paulo anaonesha  namna Ibrahimu alivyo amini Neno la Mungu, ahadi ya kupata mtoto. Na hiyo ni imani kubwa  ya kuamini kuzidi kiasi  cha matumani hayo. Kwasababu  ni jambo  ambalo lilikuwa kinyume  na hali yake alivyokuwa, kwasababu  yeye alikuwa tayari mzee na mke wake alikuwa mgumba.

Kwa kuamini ahadi hiyo Abrahamu  alianza safari , na kukubali kuacha nchi na mali zake na kuwa mhamiaji, akiwa na mategemeo ya jambo “lisilowezekana” ahadi ya Mungu ya kumpatia mtoto, pamoja na kuwa mke wake alikuwa tayari ni mgumba na mzee. Abrahamu aliamini na imani yake ikamfungulia matumaini, na kuongeza, ukifikiria kwa mtazamo wa kijujuuu jambo hili halina maana , kwasababu inaonekana kweli ni jambo lisilo wezekana. Papa aliendelea , lakini matumaini hayo yana fungua upeo , na kukuwezesha  uote hata jambo ambalo haliwezekani na hata kufikirika. Matumaini yanakufanya uingie gizani wakati  usiotegemea  ili upate kutembea kwenye mwanga.

Lakini hiyo ni safari ngumu, papa alisema , kwani kuna kipindi ambacho hata  Abrahamu alipata wasiwasi na kukata tamaa. Lakini aliendelea  kuamini hadi  kufikia nchi aliyokuwa ameelekezwa na Mungu,japokuwa muda ulizidi  kupita bila kumpata mtoto , na tumbo la Sara lilibaki na ugumba wake.

 

Papa aliendelea  “ ndipo Abrahamu alianza kulalamika kwa Bwana; “Ee mwenyezi Mung utanipa nini hali naendelea kuishi  bila mtoto, na mrithi wangu ni Elizier wa Damasko: Tazama hujanijali mtoto ; mtumwa aliyenizalia nyumbani mwangu , ndiye atakuwa mrithi wangu. Ndipo Mwenyezi Mungu akamtokea akamwambia  Hapana mtoto huyo hatakuwa mrithi , bali yule aliyezaliwa na wewe ndiye atakuwa mrithi”


Na hapo mwenyezi Mungu akamleta nje na kumwambia tazama juu angani zihesabu nyota kama unaweza kuzihesabau, na kuongeza …. huo ndiyo utakuwa urithi waki ..Na yeye akaamini Bwana alivyo mwambia kwa haki (Mw 15,2-6)
Papa akachambua hilo na kusema,  tukio hilo lilifanyika wakati wa usiku na   nje kuna giza , na  hiyo ina maana  hata katika moyo wa Abrahamu , kuna kukata tamaa, kutokana na matatizo ya kuendelea kuamini kile kisichowezekana. Hiyo ni kwababu baba huyo ameshakuwa mzee wa miaka mingi , na kwamba jamabo hili lisingewezekana kuwa na mtoto, bali anayebaki ni mtoto wa mtumwa kuchukua urithi wake.


Hata kama Abrahamu yupo anaongea na Bwana wakati huo, lakini bado bado uwepo wa Bwana siyo kitu unafanana kuwa mbali naye, kwasababu hajaweza kutimiza ahadi ya neno lake . Abrahamu  alijisikia upweke , ni mzee,  amechoka na , kifo kinamkaribia. Je ni namna gani aendelee kuamini?
Papa anabainisha kwamba  hata hivyo malalamishi hayo ni  namna ya kuishi  imani.Pamoja na hayo yote  Abrahamu aliendelea kuamini Mungu na kutumaini  chochote bado kinachoweza kutokea.


Papa aliuliza  ni kwasababu gani Abrahamu anaendelea kulalamika , na kutafuta ahadi hizo?, Ni kwasababu , imani siyo kusema ni ukimya tu na kutufanya tukubali bila mabishano ndani ya mioyo yetu, au matumaini siyo jambo la uhakika wa kukufanya usiwe na mashaka au wasiwasi, bali Imani ni mapambano na Mungu ya kumuonyesha uchungu wetu bila  kijificha. Matumaini vilevile siyo kusema yanakuondolea hofu ya kuangalia hali jinsi ilivyo, bali ni kukubali hata majaribu hayo.


Baba Mtakatifu alisema  Abrahamu kwa imani yake anaelekeza maombi yake  Mungu ili aweza kumsaidia aendelee kutumaini. Na Bwana alimjibu kwa msisitizo wa ahadi yake,ya kwamba, mrithi hatakuwa  mtoto wa mtumwa , bali  atakuwa mtoto wake manyewe atakayetoka katika uzao wake.

Hakuna chochote kilichobadilika kwa Mungu kwasababu yeye aliendelea kurudia ahadi yake aliyo tamka  tangu mwanzo, na siyo kwamba anamtokea ili Abrahamu aweze kujiskia uhakika. Uhakika  wake alio nao ni ule wa  kuamini neno la Bwana  na kuendelea kumtumainia.
Ishala aliyo mpatia Abrahamu  ni kama sala ya kuendelea kuamini na kutumainia  kile alichomwambia “ hapo mwenyezi  Mungu akamleta Ibrahimu nje na kumwambia  “Tazama   mbinguni , zihesabu ; Hivyo ndivyo wazao wako watakavyokuwa wengi.”(Mw 15,5)  Baba Mtakatifu alieleza jambo hilo  lilikuwa bado ni  ahadi na ambayo alipaswa kusubiri kwa wakati ujao.


Aidha Baba Mtakatifu alisema nini maana ya hema akisema; Mungu alimpeleka Abrahamu nje ya hema , ina maana ya kumtoa katika maono yake finyu , na kumuonyesha nyota;  aliongeza, ili kupata kuamini, inabidi  kutazama kwa macho ya imani; ni nyota tu ambazo wote tunaweza kuona , lakini kwa Abrahamu nyota hizo lazima zigeuke kuwa ishala ya uaminifu wa Mungu.

 

Na mwisho akasema baba Mtakatifu , Na hiyo ndiyo imani ,  ndiyo njia ya matumaini ambayo kila mmoja wetu anapaswa kuikimbilia. Iwapo hata sisi tutakuwa na fursa ya kutazama zile nyota , utakuwa ni muda wa kumwamini Mungua na hakuna jambo lililo zuri zaidi ya hilo.


BAADA YA KATEKESI YA PAPA


Baada ya Katekesi yake Baba Mtakatifu aliwasalimia watu wote   hasa kwa namna ya pekee vijana, wagonjwa, na wana arusi, akisema  leo ikiwa Kanisa linaadhimisha Sikukuu ya watoto mashahidi , kwa ,aombezi yao wapate kuwasaidia wote  kuwa na nguvu ya imani , na kumwangalia mtoto wa Mungu , ambaye kwa fumbo la kuzaliwa kwa Bwana amejitoa kwa binadamu wote.


“Vijana wote mtambue ya kwamba mnakua kama yeye na hivyo ni kuwatii wazazi na kuwa tayari kutambua  na kufuata utashi wa Baba aliye mbinguni”.
Akiwageukia wagojwa  baba Mtakatifu aliwatakiwa matashi mema ya sikukuu hizi za kuzaliwa kwa Bwana na hasa wao waweza kuangazwa na Mwanga wa Betlehemu , na kutambua maana ya mateso yao.


Vilevile wanandoa alisema waweze kudumisha kila siku na kujenga familia zao kwa upendo na kujitoa  sadaka zaidi.

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican








All the contents on this site are copyrighted ©.