2016-12-27 16:45:00

Watu wa Hong Hong wanapenda kukutana na Bwana hata kama wengine siyo wakristo



 “Kanisa linawapokea wale wanaopenda  kumkaribia Mungu wakati wa Sikuu ya kuzaliwa kwa Bwana” Ni utangulizi wa Maneno ya Padre Sergio Ticozzi Mmisionari wa Pime Huko Hong Kong China akitoa ushuhuda wa watu wake wakati wa mahojiano  na mwandishi wa habari wa Radio Vatican juu ya sikukuu ya kuzaliwa kwa Bwana.


Anasema; Kwa kawaida  China wanasheherekea sikukuu kwa namna ya pekee, kwasababu ni watu wengi wanakwenda kanisani, haijalishi hata kama idadi kubwa siyo wakatoliki na wala wakristo.Wanakwenda kwa kujisikia wana mahitaji; Ni  mahitaji ya kiroho ya kukutana na Bwana  , kwa njia hiyo ni fursa kubwa kwa Kanisa la Chiana kukutana na watu hawa walio na utashi wa dini , kwa imani yao katika Bwana.


Aidha alisema sikukuu ya kuzaliwa kwa Bwana imeangukia muda mfupi wa kumalizika mwaka wa huruma, ambao umekuwa mwaka wa aina yake, kwani umeleta maridhiano ya watu kwa Bwana , ya ndugu , ya jumuiya na ndani ya familia.


Halikadhalika  kwa upande wa Hong Kong, ushuhuda  wameweza kuutoa  kwa njia ya jumuiya  ndogo za kiparokia ambao wamekwenda kuwatembelea wagonjwa hopitalini, katika nyumba za  wazee , na pia vituo vya walemavu kwaajili ya kuwapelekea zawadi ndogo na kusali nao kwa kutumbuiza  nyimbo… huu ni mshikamano wa kuweza kushirikishana furaha ya Noel , ambayo ndiyo maana yake, alisema Padre Sergio.


Na hii ni kutokana na  mwaka huu  kwa namna ya pekee wa mwaka wa huruma ulikuwa na vigezo vya matendo ya huruma na kwa njia hiyo umewafanya watu kuwa na msukumo na mwamko wa kufanya matendo ya huruma ya kuwasaidia wenye shida , waliobaguliwa , wagonjwa na walio na upweke.

Akiongelea juu ya matatizo yalipo katika Kanisa la China alisema kuwa ni kumwachia yote  Bwana  anayeweza kugusa mioyo : wanachofanya wao na jumuiya zao ni kumuomba Bwana awafanye waendelee kuwa chombo cha amani katika mikono yake, na mwisho wake  hasa wapate kuwa tayari kukabiliana na vishawishi vya ulimwengu huu vinavyojitokeza.

Halikadhalika wawe tayari kufungua miyo yao kiroho kwaajili ya maelewana na watu wengine , katika jumuiya , na kuishi kwa maelewana ndani ya familia na ndani ya jamii. Hayo ndiyo matazamio ya msingi wa watu wa Hongo Kongo na China.

 

Sr Angela Rwezaula

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.