Tarehe 21 Desemba 2016 Baba Mtakatifu Francisko alikutana na Kardinali Angelo Amato Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa kwaajili ya kuwatangaza wenye Heri na watakatifu.
Katika mkutano wao ametoa ruhusa ya kuwatambua na kuwatangaza watakatifu,na wenye
heri wafuatao:
— Mwenyeheri Faustino Miguez, Padre na Mtawa wa Shirika la Masikini wa Mama wa Mungu
kwa jina jingine (Scolopi),na mwanzilishi wa Shirika la watawa wa kike (Calasanziane
) wa watoto wa Mungu mtume; alizaliwa 24 machi 1831 na kifo chake 8 machi 1925;
— Mtumishi wa Mungu Leopoldina Naudet, Mwanzilishi wa Shirika la watawa wa kike
wa Familia Takatifu ; alizaliwa 31 mei 1773 kifo chake 17 agosti 1834.
— Mashahidi wa watumishi Mungu Matteo Casals, Padri na mtawa , Teofili Casajús, mwanafunzi
wa nadhiri, Ferdinando Saperas, ndugu aliyefunga nadhiri , na wenzao 106 wa Shirika
la Wamisionari wa watoto wa Moyo safi wa Bikira Maria; waliuwawa kwa chuki ya
kutetea imani yao wakati wa vita ka ya mwaka 1936 na 1937;huko Hispania.
—Mtumishi wa Mungu Giovanni Battista Fouque, Padri wa Jimbo ;aliyezaliwa il 12 septemba
1851 na kifo chake 5 desemba 1926.
— Mtumishi wa Mungu Laurent wa Roho Mtakatifu (enzi zile : Egidio Marcelli), mtawa
wa Shirika la la Mateso ya Yesu Kristo ; aliyezaliwa 30 agosti 1874 na kifo chake
14 oktoba 1953;
— Mtumishiwa Mungu Maria Raffaella wa Moyo Mtakatifu wa Yesu (wakati ule : Sebastiana
Lladó y Sala), Mwanzilishi wa Shirika la Wanisionari wa Mioyo ya Yesuna Maria; aliyezaliwa
2 Januari 1814 na kifo chake 8 machi 1899;
— Mtumishi wa Mungu Clelia Merloni, Mwanzilishi wa Shirika la mitume wa Moyo Mtakatifu
wa Yesu ; aliyezaliwa 10 machi 1861 kifo chake 21 novemba 1930;
— Mtumishi wa Mungu Isidoro Zorzano Ledesma, mlei , wa Shirika la Msalaba Mtakatifu
na Opus Dei; aliyezaliwa 13 septemba 1902 na kifo chake 15 Julai 1943.
Sr Angella Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.
All the contents on this site are copyrighted ©. |