2016-12-22 13:44:00

Mwaka 2016 waandishi wa Habari 74 wamepoteza maisha yao vitani na serikali za kimabavu


Undishi wa habari ni taaluma iliyo hatari , leo hii ni nchi nyingi duniani  kote, si tu katika maeneo ya vita yenye Serikali za kimabavu , bali pia katika mazingira juu ya karatasi, na demokrasia.
Hii ni Ripoti  ya mwaka ya Shirika la Waandishi wasiokuwa na Mipaka, wenye makao  Mjini Paris Ufaransa na Kamati ya Kulinda Waandishi wa Habari mjini New York.


74 wafanyakazi wa vyombo vya habari  wamepoteza maisha yao ikiwa , 57 ni waandishi wa habari, 9 ni  wanablogu na 8 wasaidizi wa  vyombo vya habari kwa  mwaka 2016, na hiyo ni sababu ya utendaji wao wa kazi wa kutoa taarifa tu. Sehemu kubwa wa waandishi wa habari waliopoteza maisha katika sehemu za vita :19 Siria, 10 Afghanistan, 7 Irak na 5 nchini Yemen.Lakini katika nafasi ya tatu kwenye orodha ya mstari mwekundu kwa uchapishaji  ni nchi Amerika ya kusini katika nchi ya Mexico ambapo 9 ni waathirika wa tukio hilo. .

Shirika la Waaandishi wasio kuwa na Mipaka wanalalamika kuwa kuna mapengo ya kweli ya maelezo   japokuwa waandishi wa habari 780 wamepoteza maisha yao kwa kipindi cha  miaka 10 iliyopita wakiwa wanatafuta hali halisi na siyo tu ya vita vinayoendelea ,bali juu ya uhuru na  ukiukwaji wa haki, rushwa, vitu ambavyo ni changamoto na  ni kipigo hata kwa nchi nyingi za kidemokrasia.

Kutokana na  takwaimu kwa mfano nchi ya Italia kwa upandewa wa Shirika la Ulaya la haki za binadamu zinaonesha, miezi tisa ya kwanza ya mwaka 2016, 92 yamekuwa ni matukio ya vitisho, mashinikizo na  mashambulizi dhidi ya waandishi wa habari,ikifuatia nchi ya Ufaransa ambayo ilipata matukio 95.


Mwaka 2016 vilevile umekuwa mwaka mbaya zaidi kwa kufungwa jela waandishi wa habari , kama isemavyo Kamati ya ulinzi wa Waandishi wa habari (CPJ) Ni waandishi 256 walioko ndani ya magerreza za Serikali. 81 wakiwa nchini Uturuki, na zaidi ni waandishi 38 walioko magereza ya China, ikifuatiwa  na nchi tatu za Afrika ambazo ni  Misri , Eritrea na Ethiopia. Mbali na waandshi hao , bado waandishi 40 waliopotea au kutekwa nyara katika Mashariki ya Kati na Afrika ya Kaskazini.

 

Sr Angela 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican








All the contents on this site are copyrighted ©.