2016-12-22 13:23:00

Bangladesh: Makanisa 62 ya kikristo kulindwa wakati wa sikukuu ya kuzaliwa kwa Bwana


Baadhi ya viongozi wa Kikristo wa  Bangladesh walikutana  na Waziri wa Mambo ya Ndani na  kuomba serikali  kuhakikisha usalama wa Wakristo wakati wa kipindi cha sikukuu ya Kuzaliwa kwa Bwana na Waziri aliwahakikishia  ulinzi wa polisi kwa  makanisa 62 katika mji mkuu.


Mkutano huo ulifanyika katika ofisi ya Waziri  wa Mambo ya Ndani huko Dhaka, na wawakilishi 25 wa Muungano wa Makanisa ya Kikristo .Naye Rais wa Muungano wa Wakristo  Nirmol Rozary aliliambia shirika la habari  la AsiaNews akisema ,"walikutana na waziri huyo na walimpelekea heri na salamu ya sikuu ya kuzaliwa kwa Bwana kwa niaba ya Jumuiya zote za  Kikristo.


Aidha akielezea hali hiyo aliendela na kusema ,wasiwasi wa wakristo unatokana na hali ya kutokuwa wavumilivu  wa wageni kutoka nchi za nje walioko katika nchi na hasa Mapadre,pia  Jumuiya ndogo za Kikristo na wahindu.Kiongozi huyo wa  Wakristo aidha alimuomba waziri mambo ya ndani kuhakikisha uwepo wa umeme  bila kukatika watakapokuwa wanasali misa za sikukuu .

Na kwa upande wa Waziri Asaduzzaman Khan Kamal aliwahidi  kuwa hatakikisha hatua zaidi za usalama zinatekelezwa nchini kote wakati wa sikukuu za Noel na mwaka Mpya, na kuongeza ya kuwa tunao wasiwasi juu ya ulinzi wa Wakristo , polisi wetu watakuwepo katika makanisa yaliyopangwa kwenye vipindi hivyo vya sikukuu ya kuzaliwa kwa Bwana


Mji wote utadhibiti makanisa 62 na kuahkiksha kwamba nchini kote unawekwa mifumo ya ufuatiliaji wa mitambo ya kulinda  na pia kuzuia  foleni za magari kupitia barabara  ya  maeneo ya Ibada za kikristo.Hata hivyo Serikali imewataka  pia wakristo wasifanye sherehe kwa kutumia milipuko ya  fataki .
Huko Bangladesh wakristo ni wachache, asilmia 0,6% ya  milioni 160 ya wakazi.Na Jumuiya ya wakristo iliyo kubwa ni ile ya wakatoliki, ambao wanakaribia waamini 600,000.

 Sr Angela Rwezaula. 

 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican
 

 








All the contents on this site are copyrighted ©.