Vita na matumizi ya nguvu kamwe hayakuweza kuleta amani na haki , bali zaidi ni kuleta vurugu, vifo na uharibifu, hayo yalitamkwa na Na askofu Mkuu Pierbattista Pizzaballa katika mkutano na waandishi wa habari juu ya tukio la sikuku ya kuzaliwa kwa Bwana Jumanne 20 Desemba 2016 huko Yerusalem, na Mons. Pizzaballa ni msimamizi wa kitume wa nchi Takatifu huko Yerusalemu.
Msimamizi huyo alisisitizia juu ya kutaka wafanye mazungumzo ya kisiasa na kupata
na ufumbuzi kwani aliendelea “Jeshi linaweza kushinda vita , lakini katika ujenzi
inahitaji sera za kisiasa, na sisi hatuoni , na maisha ya wengi yako hatarini katika
mchezo wa vita, na mwisho wake masikini na wanyonge ndiyo wanaotoa gharama kubwa.”.
Katika hotuba yake msimamizi wa Kitume Yerusalem alitoa mfano miongoni mwa jumuiya
za wakristo wa misiri , kwamba wanaishi chini ya vitisho , kama ilivyodhibitisha katika
mashambulzi ya hivi karibuni katka Kanisa la kikopt mjini Kairo.Aidha na kusema, hata
sisi ni sehemu ya uwajibu, kwani hatuwezi kuendelea kuongea daima juu ya mazungumzo
, haki na mani. Maneno matupu hayatoshelezi, tunatakiwa kupambana kwaajili ya umasikini
na haki , kwa kutoa ushuhuda wa huruma.”
Hali kadhalika alisema juu ya mashambulizi ya nchi kuanzia Yordania ambapo Jumapili
iliyopita ilitokea mashambulizi ya kigaidi huko Karak na kusema hata huko virusi vya
magaidi vimeingia kwani siyo habari mpya , ni lazima kufanya kazi sana hasa katika
sehemu ya elimu na maendeleo, la sivyo hata katika sehemu hiyo vijana nao watajifunza
ugaidi kama wao.
Askofu Mkuu pia alilaumu juu ya ukosefu wa maono, ya nchi ya Israel na wapalestini
ambao kwa muda mrefu wamekosa mazungumzo na dhamira dhabiti ya amani na kusema ni
jambo ambalo watawala wanapaswa kuliangalia kwa haraka na kwa ujasiri , kwaajili
ya kusaidia watu wao wanaokabiliwa na hali ngumu na wanazidi kuomba amani.
Sr Angela Rwezaula
Idhaa ya Kiswahili ya radio Vatican
All the contents on this site are copyrighted ©. |