2016-12-19 14:40:00

Huduma kwa watoto na wazee ni kuendeleza historia na hekima ya maisha


Jumamosi 17 Desemba 2016 Baba Mt.Francisko Alikutana na wanajumuiya ya Nomaldelfia mjini Vatican nakuwaeleza, anayo furaha ya kukutana na kutaka kujua uzoefu wa Jumuiya yao, na kwamba alishangazwa juu ya ushuhuda wao. 
Katika hotuba yake aliwaeleza , kipindi cha majilio kinatusaida kutafakari juu ya maajabu ya Mwana wa Mungu aliyekuja kwa njia ya mwili na katika kuzaliwa kwake ameleta mwanga na amani duniani.


Sikukuu ya kuzaliwa  kwa Bwana ni kuonesha Mungu aliye juu na ambaye anatawala ulimwengu nni yule aliyejinyenyekeza katika udhaifu wa mtoto. Aliendelea, hii inatufundisha tusijiweke mbele zaidi ya wengine , bali tumeitwaa kujishusha na kuwa wadogo  ili kuwahudumia wengine walio wadhaifu. Na hii ni kusema kwamba kama  Mungu mwenyewe kwa njia ya mwanaye alikuja duniani kama binadamu tulivyo  sisi ila hakuwa na dhambi ni sawa na kusema , kwa maneno yake  Yesu , “chochote mlichowatendea wadogo mmenitendea mimi” (Mt, 25,40).


Papa aliendelea mwanzilishi wenu Padre Zeno Saltini alitambua hayo , lakini pamoja na matatizo aliyokutana nayo alikwenda mbele  kwa matumani, kwa lengo la kupeleka mbegu ya Injili hata katika sehemu zenye zenye ugumu wa kupokea.Akaongeza; na aliweza! Kwasababu hiyo Jumuiya yenu ya Nolmadelfia ni mfano huo. Padre Zeno leo hii anawakilisha  mfano wa imani ya kitume kwa Kristo na  ameigiza mwalimu wake ambaye ni  Mungu. Na huyo anaendelea kuinama   kwa watu wanoteseka, wadhaifu  na masikini wa mwisho.
Hivyo ushuhuda wake, uwaongoze kila siku katika kutoa matunda  ya wema na kupanda  mbegu  inayoongozwa na upendo wa kiinjili , na kwa uaminifu wa Kanisa.


Aliwakumbusha tena maneno ya Yesu, ya kuwa “ kuwalisha wenye njaa, kuwavalisha walio uchi , kuwapokea masikini kati ya watu, ni sawa na kupokea  na kumpenda Mwana wa Mungu, bali  atakaye fanya kinyume na hayo atakuwa kama  asemavyo Mt. Yohane ya kuwa kama umpendi ndugu yako unaye muona , unawezaje kumpenda Mungu usiye muona(1Yh 4,20).


Alimalizia hotuba yake kwa wanajumuiya hiyo ya Normadelfia akisema,  ndugu kaka na dada urithi wenu wa kiroho , unahusiana  kwa namna ya pekee na maisha ya kindugu, yenye sifa hasa ile ya ukarimu kwa watoto na kutoa huduma  kwa wazee. Ninawatia moyo wa kuwapa  mifano jamii juu ya huduma hiyo muhimu. Ya watoto na wazee kwajili ya kujenga maisha yao ya baadaye kwa watu; kwani watoto wataendeleza mbele  historia yao, na  wazee kwasababu wao, utoa uzoefu  na hekima ya maisha yao.


Papa alisisitiza ya kwamba wasichoke kamwe kuendeleza majadiliano haya kati ya vizazi , na kulifanya neno la Mungu kuwa ndiyo msingi wa maisha kamili ya kila siku. Kwa namna hiyo mtakuwa mfano wa karibu wa Mungu kati ya watu nakuweza  kuzitambua nyuso za wale wadhaifu ya kwamba ni mfano wa mtoto yesu. Na aliwatakia sikukuu njema wote ya kuzaliwa kwa Bwana na kuwabariki

 

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican

 








All the contents on this site are copyrighted ©.