2016-12-13 09:38:00

Barua ya Papa Francisko kwa Rais Bashar Al Assad wa Siria


Baba Mtakatifu Francisko kwa kumteuwa na hatimaye kumsimika Askofu mkuu Mario Zenari kuwa Kardinali, alitaka kuonesha kwa namna ya pekee, upendo wake kwa wananchi wa Siria ambao kwa takribani miaka mitano wamekuwa wakiteseka kutokana na vita. Baba Mtakatifu kwa njia ya Kardinali Mario Zenari, Balozi wa Vatican nchini Siria amemtumia barua Rais Bashar al Assad, akimwomba pamoja na Jumuiya ya Kimataifa kusaidia mchakato wa kusitisha vita nchini Siria kwa kujikita katika mchakato wa majadiliano yatakayosaidia kurejesha tena maridhiano kati ya watu kwa kuondokana na chuki na fitina kati yao.

Baba Mtakatifu analaani misimamo mikali ya kidini na kiimani kwa kumwomba Rais Bashar Al Assad kuhakikisha kwamba, sheria za kimataifa zinaheshimiwa mintarafu ulinzi na usalama kwa raia pamoja na kuhakikisha kwamba, waathirika wanafikiwa na misaada ya kimataifa!

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.

Idhaa ya Kiswahili ya Radio Vatican.








All the contents on this site are copyrighted ©.